![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjGLwRn97RqJ5uejqVsqx225DOanAiMF3djwo9JQ7GxUkUoMN8nRUmxfi1VXbOl4DdZyompJrj6yrsnkOj1kSpV-ICHGVqlPTjnS3YNVs_tKeBynWkl7BDfzzJPRj_yU0V7O2tZazdUhB4/s320/4057_d004_00629_r.jpg)
utoto upofu,
huyaoni ya dunia,
hupenda unyoofu,
yakipinda huchukia,
utoto mapungufu,
wazazi huvumilia.
utoto kumbe ni hivi,
mama yangu nisamehe.
nisamehe mama yangu,
hakika nilikuudhi.
enzi za utoto wangu,
sikuitaka ajizi
nilipotaka jambo langu
ulipaswa kulikidhi,
sikuyajali machungu
poleni sana wazazi.
poleni sana walezi,
nyie adha mwazijua
nimekua siku hizi
namie nayatambua,
mgumu sana ulezi,
watoto wanasumbua
hasa wasiku hizi,
utajuta kuwajua.
Utajuta kuwajua
watakacho ndicho hicho
werevu wasotambua
kama huna ama unacho
wataanza kulilia
ukileta kiinimacho
wamezaliwa wanajua
hawataki danganya toto.
mabingwa wakuchagua
kipikwe chakula gani,
nawewe utaangalia,
wakitazama katuni,
mada zao kuchangia
itakupasa ukiwa nyumbani.
wao ndio hudatia
nyumba yote nje ndani.
niwao ndio mabosi
wewe kijakazi wao,
kukusaidia kazi
ni mpaka hiyari yao
haweshi ulalamishi
wakitaka jambo lao
utoto kweli ni ukwasi
ukata umbali nao.
nikama vile wanajua
ufalme wote niwao.
haweshi kujitanua,
utoto kwao ni ngao.
hutumia kulia lia
kupata walitakalo.
maisha yametimia
kwao siyo hua ndio.