UONGO WA MAMA 'ANGU

Ni Simulizi niliyoitohoa kutoka kwenye clip flani iv yakizungu.

Nimeweka Utashi wangu ili kufikisha ujumbe kama uliokuwepo kwenye clip ile, sijacopy nikapaste, kuna vingi nimebadili kuleta uhalisia...

Na.
Omar Zongo

"Usihuzunike, sihisi maumivu, najiona nina afadhali!"

Huu ndio ulikuwa uongo wake wa mwisho kuniambia!!

Baada ya hapo alifumba macho na hakuweza kufumbua tena.

Roho yake ikaacha mwili!

Leo ndio nakumbuka, mama yangu alikuwa Muongo, hata kabla ya siku hii ya mwisho.

Nakumbuka, wakati mdogo, mara nyingi chakula chetu kidogo kinachopatikana, yeye alikuwa hali na alikuwa akisema

 "nimeshiba kijana wangu, kula wewe ushibe!"

Nilikuwa namshuhudia akiokoteza mifupa ya samaki niliyobakisha mimi.

Hata nilipokuwa nikimbakishia minofu ya samaki alikataa kabisa akisema hapendi samaki!!

Nilipoanza shule ya awali, ilimbidi afanye kazi mbilimbili ili aweze kumudu ada za shule.

Hakupata muda wakupumzika!

Mara zote nilipokuwa nikishtuka usiku nilimkuta bado anafanya kazi za watu! Maskini mama alifanya kazi usiku na mchana, Hakuwa na muda wakupumzika.

Nilipokuwa namwambia "mama nenda kapumzike, kesho utamalizia kazi zako" alinijibu huku anatabasamu "sina usingizi mwanangu, we lala tu"

Maisha yetu yalizidi kuwa magumu baba alipofariki!!

Mjomba 'angu alimshauri mama aolewe tena lakini mama akakataa, alihofia labda nitabaguliwa na huyo baba mwengine.

Alisema "sitaki mapenzi"

Hapa pia mama aliongopa.

Hatimaye nikamaliza chuo!!

Nikiwa Na kazi nzuri yenye posho Na mshahara mnono, niliona ndio wakati sahihi wakuishi na mama angu kwa furaha.

Lakini nilipomgusia suala hilo alipinga akasema "hapana kijana wangu, mimi nitaishi kwangu tu! Najisikia furaha zaidi nikiwa hapa"

Alitaka niwe huru, nifurahie maisha yangu!

Miezi michache baadae mama 'angu akaanza kuumwa!

Hospitali wakabaini ana kansa ya tumbo!!

Alidhoofu mno! Afya yake ikanywea, akawa dhaifu kwenye kitanda cha hospitali.

Kama mtoto wake pekee niliweza kuyahisi maumivu yake.

Nilikuwa namsogelea kwa upendo! Nikishindwa kuyazuia machozi yangu yasimdondokee mwilini mwake.

Lakini bado mama angu, akiwa Na nguvu chache zilizobaki mwilini mwake, alitabasamu na kisha kusema

"Usihuzunike, sihisi maumivu, najiona nina afadhali"

Nakumbuka vizuri.

Sauti yake iliyotamka maneno hayo ndio ya mwisho kuisikia.

Aliniongopea yuko sawa, muda wote alitaka kuniona mimi niko kwenye furaha.

Alinijali mimi kwanza huku akiwa tayari kuficha machungu yake!!

Uongo wake ulisindikiza upendo wake mkubwa kwangu!!

Kama yeye ninani!??

Muda huu Viganja vyangu vinachezea udongo wa kaburi lake, machozi yangu yakidondokea mgongo wa nyumba hii isiyo na mlango.

Akili inashindwa kuamini nahisi bado ananiongopea!

Nahisi bado yupo mahali kwenye hii dunia!.

SIMULIZI ZINAISHI.

ANDIKO TATA

Na.
Omar Zongo

Hili ni andiko Tata tena tupu, linalosindikizwa na ala ya simanzi!

Linajichora kwa kalamu ya ukiwa kwenye karatasi ya upweke.

Andiko lenye nukta ya kilio na koma ya kukata tamaa!!

Andiko lenye madoa ya machozi na uchakavu wa kilio.

Mwandishi nimie mkiwa mwenye tamaa ya nuru, niliyesimama njia panda mbele kiza, nyuma miba, kulia moto, kushoto mamba mwenye njaa!

Mwandishi mchovu mwenye akili ya majuto! Kosa langu silijui lakini najihisi nina hatia.

Duniani wakumlaumu nadhani nimimi mwenyewe!!.

Naandika ilhali nina uchovu ila kwa vile ukamilifu wa Andiko nautaka siachi kujihimu niendelee ingawa kwi kwi za kilio zanikosesha umakini.

Ni ipi tamati ya Andiko!! Je ni kusagwa na meno ya mamba au kushambuliwa na ncha za miba???

Je, nikupata joto Kali la moto au kupotelea kizani!??

Ninani msaidizi katika hatua yangu ijayo???

Ninani mpatanishi wa mgogoro wa nafsi yangu!??

Je nimimi mwenyewe au kudra za Mungu!??

Je ni rafiki ambaye simuoni au ndugu akiyenikimbia!?? Je ni Mpenzi wakufikirika au mwanangu aliye mbali??

Ni ipi hasa hatma ya Andiko??

Ni kaburini kwa kuzikwa au kwa kujizika mwenyewe!! Eti ni Ipi Tamati ya Andiko?

Andiko lenye utata uliogubikwa na upweke!.

Nani wakumuonesha alihariri Andiko, kabla halijasomwa Na wengine  usahihi ujazane.

Nataka kichwa tulivu chakung'amua andiko, kisiwe na upungufu wakutatua magumu.

Maneno yalo adhabu yakemewe kwa busara, yaletwe kwenye wepesi waelewe walo lala.

Andiko masikini ubini wake dhalili, mwandishi hali duni, unga mwana, dhoflehali.

Ala yake majonzi, yarindima kwa kilio, yanadi upweke mwisho wake jaribio.

SIMULIZI ZINAISHI