SEHEMU YA 1&2

SEHEMU YA KWANZA


''Ni kawaida kwa hadithi nyingi pendwa kuwa na sehemu ya kwanza na sehemu ya pili na nyengine nyingi zenye mfululizo wa visa vya kusisimua, lakini ukweli wa mambo ni kuwa hali ni tofauti katika mapenzi, Hadith ya mapenzi inayonoga zaidi ni ile ya sehemu ya kwanza, ukiiharibu kwa kudhani kuwa utapata sehemu ya pili ni kosa kubwa sana ni sawa na ufa usioweza kurekebishika''

HII HADITH HAINA JINA INAITWA SEHEMU YA KWANZA NA SEHEMU YA PILI.....
NI KISA CHA MAPENZI .....

Na
 Bin Zongo
 
Mapenzi yamekolea hakuna aliyeona kero kwa mwenzie, kila mmoja anaishi kwa amani na hutabasamu kila wakati akikumbuka uwepo wa mwenzake.

marafiki zao walikuwa wanawaona machizi mana walipokuwa mbalimbali kila mmoja alikuwa busy na simu yake akichart na mwenzake nakucheka cheka kila saa kama chizi mpya aliyepelekwa kituoni kwa matibabu.

mapenzi yao yalikuwa yanavutia kama mapenzi ya kitabuni, yalifanya kila mmoja kati yao aone thamani yakuzaliwa kwake,

nafsi zao zilisonona kila zilipokumbuka kifo, hakuna aliyekuwa tayari kumuacha mwenzake maombi yao siku zote yalikuwa wafe wakiwa wote...ni nadra kutokea lakini walitamani sana kifo chao kitokee wakiwa wamekumbatiana!

mapenzi ya dhati yaliumbwa ndani ya mioyo yao! niseme nini mimi kudhihirisha namna walivyopendana!!!.

Raha ya mapenzi ya dhati ilidumu kwa muda mrefu kiasi hata ilipotokea mwanaume amebadilika tabia hakuna aliyeamini!.

lakini ukweli ulikuwa huo, jamaa alianza tabia ngeni kabisa.

alianza ubinafsi wakujiamulia mambo yake, alipanga ratiba zake bila kumuhusisha Bishosti.

tafakari wewe ni maumivu kiasi gani umpendae abadilike ghafla namna hii ilikuwa ni tanzia. hakuna aliyemudu kufuta chozi la bishosti.

kilio chake kilizidi kile cha msiba wa bibi yake mzaa mama ambaye walikuwa wakiitana shoga.

Bishosti alijuta kufahamu mapenzi ile taamu sasa iligeuka shubiri hakuna neno baya tena alilopata kulisikia duniani kama Mapenzi.

mtu aliyeyaita mapenzi ni Upuuzi aliona kama bado anayasifia yeye aliyafananisha na Jinamizi litembelo usiku kutafuta roho za wapendanao.

Bwanamkubwa alibadilika simu yake ilikuwa ni kawaida sasa kutumika hata usiku wa manane huku swali anaongea na nani akiwa halitaki kutoka kwa Bishosti.

kama ni maji yalimfika shingoni Bishosti taratibu akaamua kujifunza kuwa mbali na Bwana mkubwa.

ilikuwa ngumu lakini angefanya nini na bwamkubwa keshaamua?

utengano wao ulikuwa ni wa bila kuambiana TUACHANE sasa kila mmoja akawa na maisha yake. no simu no salamu. walipotezeana kwa herufi kubwa kabisa huku maumivu makuu yakiwa yametanda zaidi mauongoni mwa Bishosti.

siku, wiki na hatimaye Miezi ikapita.

Nani alikwambia penzi la historia kufutika mioyoni mwa wapendanao ni rahisi?

Bwana mkubwa nafsi ikaanza kumsuta! lawama ndani yake zikaanza kurindima, alijituhumu kuwa mkosefu mkubwa.

hamu ya mpenzi wake ikarejea kwa mabavu ikimkaba koo sambamba na shutuma kibao za kwanini amtenge mwanamke aliyekuwa akimpenda kwa dhati.

kuna siku moja Usiku  bwanamkubwa alishindwa  kabisa kuumaliza yaani hakubahatika kutembelewa kabisa na usingizi, alijikuta anatamani sana uwepo wa Bishosti.

mwanzo alidhani masikhara ila mwisho uzalendo ukamshinda usiku uleule
akaitafuta simu yake nakuisaka namba ya Bishosti akaipiga kwa unyonge akiomba msamaha akihitaji penzi lirudi tena..

mishale ya saa ilikuwa ni saa nane za usiku bila shaka shetani aliyeharibu penzi lao alikuwa kajisahau na amelala fofofo, hivyo bwana mkubwa pamoja na bishosti wakatumia fursa hiyo kurudiana.

LAKINI KUMBE NI HERI UFA WA UKUTA WA NYUMBA HUREKEBISHIKA LAKINI UFA WA UKUTA IMARA WA PENZI KAMWE HAUREKEBISHIKI....IlE LADHA YA PENZI LAO LA MWANZO WALIJITAHIDI KUIRUDISHA LAKINI WAPI!


KUMBE BI SHOSTI ALIRUDI KWA BIMKUBWA SABABU YA MAZOEA TU ZILE SIKU WALIZOKUWA WAMETENGANA TAYARI ALISHAMPATA MWENGINE.....HEBU FUATANA NAMI SEHEMU YA PILI KUJIFUNZA ZAIDI UJUE MAPENZI NI NINI....

  SEHEMU YA PILI


Ucheshi wa bishosti, ukarimu, utani na kucheza pamoja ndiyo vitu vikubwa vilivyomfanya Bwanamkubwa atake kurejeana na Bishosti.

mwanzo alijidanganya kuwa anaweza kuachana na bishosti kirahisi na kusiwe na tatizo lolote lakini nafsi ilimsuta hakuona mwanamke wakutengeneza nae historia zaidi ya bishosti wake.

aliomba msamaha akitaka penzi lao lirudi tena, bishosti alikubali lakini tayari alishatafuta faraja kwa jamaa mwengine lakini angefanya nini wakati ni ukweli kwamba muda mwingi akiwa na jamaa alikumbuka uwepo wa bwanamkubwa?

bishosti aliyajua maumivu ya mapenzi na alijua jinsi yanavyotesa mioyo ya watu, kila alipokumbuka alivyoteseka hakuwa tayari kabisa kumuumiza kijana wa watu hivyo hakutaka kumuacha mpenzi wake mpya aliamua kutumikia mabwana wawili.

pengine hilo ndilo lililoleta kasoro kwenye penzi lake na bwanamkubwa,

historia yao ile ya sehemu ya kwanza ilibaki kuwa historia kweli, sehemu ya pili ya penzi lao ilikuwa ni tofauti kabisa.

bishosti alikuwa mkali na simu yake, alificha maovu yake, bwanamkubwa alibaki na tahamaki huku akijilaumu kuwa yeye ndiye chanzo cha yale yote.

bishosti alikuwa mpole sana kwa bwanamkubwa lakini safari hii alimuchukulia kawaida tu bwanamkubwa na alikuwa tayari kabisa hata baadhi ya vitu kumkatalia.

"hakika bahati kurudi mara mbili katika mapenzi nayo ni bahati"

mara zote bwanamkubwa alikuwa akijiwazia maneno hayo kichwani mwake alipokuwa akiyaona mabadiliko ya mpenzi wake.

alirudi nyuma kimawazo nakukumbuka kuwa alitumia muda mrefu sana kulijenga lile penzi la sehemu ya kwanza na aliumia zaidi kuona hawezi tena kumfanya bishosti kuwa yule wa mwanzo.

Kwa mara ya kwanza kabisa bwanamkubwa aliyaona makosa yake akajifunza kutumia vema nafasi aipatayo kwa maana nafasi kurudi tena ikipotea ni ngumu.

alijiona pia kuwa ni mume bora baadae kwa mkewe atakayempata sababu hatamdharau nakumuumiza kama alivyofanya kwa bishosti, aliona hapaswi kuendelea kuwa mtumwa kwa biahosti ambaye alisamehe kwa mdomo lakini hakuwa tayari kuenzi mapenzi kwa moyo wake wote wa mwanzo.

kwa mara ya pili wakaachana tena safari hii wakiambiana TUACHANE baada ya bishosti kudanganya anaenda kulala kwao kumbe alienda kwa jamaa ake mwengine.

bwanamkubwa aligundua hili akahisi awezi kuendelea na bishosti SASA RASMI WAKAACHANA.

lakini nikwambie kitu kuhusu mapenzi ni kwamba kama ingeendelea sehemu ya tatu bila shaka BISHOSTI yeye ndio angekuwa ndiye mwenye majuto sababu katika mahusiano kinachoumiza zaidi ukiachana na mtu ni pale unapogundua wewe ndio ulikuwa mkosaji...

BILA SHAKA KUNA FUNDISHO KATIKA SEHEMU YA KWANZA NA SEHEMU HII YA PILI YA SIMULIZI HII...

"MAPENZI NI ZAIDI YA UKIFIKIRIACHO"
Bin Zongo....

MWISHO....

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »