RUDI KWA MAMA

Na.
Omar Zongo

Wino huu uliomwagika umeandikwa Na yatima asiye Na baba wala mama!

Mwenye machungu ya kumbukumbu kila atazamapo picha za wazazi wake!

Mwenye tamaa yakuzungumza Na mama kumwambia anampenda! Nakushauriana na baba jinsi dunia inavyokwenda.

Leo wino wangu umebeba dhamira yakukumbusha urudi kwa Mama.

Usiseme hakuna sababu yamsingi yakwenda kumsalimia mama!

Ukifanyacho kinakupa riziki, mafanikio na utajiri lakini vitu hivyo ni vichungu siku utakapokuwa huwaoni wazazi wako.

Siku watakapokuwa mbali Na upeo wa macho yako!

Siku nawewe utakapokuwa yatima.

Rudi kwamama!

Nenda kamwambie unampenda sana! Kaseme nae yote yakwako naumsikilize yote yakwake.

Hakikisha anafarijika kwa uwepo wako!

Usitoe hata dakika akahisi upweke! Akahisi umemtenga nakuzipa thamani kazi zako au watu wako wengine ulionao.

Kumbuka wao wanakuona wamuhimu, mwenye nguvu Na wathamani! Kwasababu ya juhudi za wazazi wako.

Walikesha nawewe ulipokuwa unawasumbua ukilia usiku kucha enzi za uchanga wako.

Walihakikisha unanyamaza haraka pindi uliponyanyua kinywa chako kulia kwa nguvu.

Muone MUNGU rafiki yangu naleo urudi kwa Mama!

Mwenzako natamani sana ule muda wakutafuta walau namba ya mama angu niipige nimsalimie.

Lakini kwenye simu yangu haipo!

Nimeifuta!

Ndio, nimeifuta tangu nilipotoka kuweka dongo la mwisho kwenye nyumba yake ya milele.

Rudi nyumbani Leo! Kama haiwezekani panga hata kesho, mama Na baba wanakusubiri!

Nafsi zao zinatafakari mauti!

Wanaona namna umri wao unavyokwenda mbele, hisia zao nikwamba wanakaribia kufa.

Nenda Leo! Utawafariji nakuwaondoa hofu walio nayo,

Watajiona wenye nguvu na wanasababu zakuendelea kuishi.

Mimi mama yangu alivyokuwepo sikuwahi kupata nafasi yakumkumbatia nakumbusu kwa upendo.

Leo hii najuta natamani siku zirudi nyuma, nimkumbatie kisha nimbusu kwenye paji lake la uso Na mwisho nimwambie nampenda sana.

Nasikitika kuwa siwezi tena kufanya hivyo ndio maana Leo nakwambia rudi kwamama.

Ukifika kule utamkuta nababa.

Wape ruhusa wakutume kama watapenda! Waambie wasiogope maana kwao hujawahi kukua.

Cheo chako kazi yako! Pesa zako vyote viache getini, ingia kwenu ukiwa mtoto kabisa.

Waazime sikio lako! Waambie nini shida Na pia wangependa wakuone vipi kwenye maisha yao yote yaliyobaki.

Fanyia kazi mawazo yao!

Hakika watahisi ni wenye kuheshimiwa sana Na wewe.

Wino wangu umeisha!

Naomba niishie hapa kwa kukwambia kuwa NINA SABABU YAKUNENA HAYA KWAKO.

SABABU YENYEWE NI UKIWA NILIO NAO KWAKUKOSA KABISA WATU WAKUWALIPA FADHILA YA KUNIZAA, KUNILEA NA KUNIONGOZA ENZI ZOTE ZA UTOTO.

Mungu awasamehe wazazi wetu waliotangulia mbele ya haki Na awape afya njema walio hai ili tuendelee kuchuma upendo halisi na muongozo thabiti.

"Hofu, wasiwasi Na mashaka niliyonayo, vinanipa sababu niseme kumbe hata Jasiri kuna vitu anaviogopa"

BinZongo...