MUHIMU KUJUA @ukweli unaumbua

Ukweli unapotaka kudhihirika kamwe hauwezi kuzuiliwa na nguvu ama utashi wowote alionao mwanadamu.

amini nakwambia ukweli una nguvu adimu ambayo haizuiliwi kamwe na vitu kama Pesa, maneno mengi, cheo, huruma wala kujuana.

Ukweli ni jambo la kuajabia maana lina 40 zake kama ilivyo kwa siku za mwizi.

Ukweli unapotaka kudhihirika haupokei rushwa wala hongo tena humchagua yoyote hata awe ndio bingwa wa uongo siku hiyo hujikuta akianika sura ya ukweli mbele za watu.

Ni ukweli pekee ndio ambao huruhusu wenyewe kufichwa lakini unapotaka kujidhihiri hujidhiri wenyewe kwa njia zake.

ukweli jambo balaa ambalo nalistaajabia lilivyokaa! maana lenyewe ndio linaruhusu kukumbatiwa na waongo tena wakiruhusu vitu kama Chuki, Uadui, Mauaji, Ubinafsi, Rohombaya na choyo vivae vazi la Upendo, Urafiki, Wema na Kusaidiana na siku ukweli ukijiachia hubaki aibu kwa watu hao waongo.

Mra nyingi sifa za ukweli huumiza na ndio maana wengi wetu hatupendi kusadiki mambo ya kweli mbaya zaidi tupo radhi kuruhusu uzushi utufurahishe kwa kuhofia ukweli utatudhoofisha.

kwasasa wakati unasoma ujumbe huu nina uhakika kuna watu mud huu wanakutana na ukweli na wanaumia lakini hawana namna ya kuupinga

sijui kama na wewe ni miongoni mwao ila hapa nitawataja baadhi tu wanaoonja dhoruba ya ukweli

1: mgonjwa hospitalini au nyumbani au hata aliye njiani kwasasa anajua mwili wake unaumwa na huo ndio ukweli wenyewe ambao kamwe hawezi kuukataa.

2: Fukara asiye na kitu nae ni miongoni mwa watu ambao wanakutana na ukweli wahali zao na wanaumia mno wanatamani vitu vizuri wavimiliki nyumba nzuri, gari na hata pesa za kujikimu, familia bora na mengineyo mataamu yakidunia lakini ukweli ni kwamba muda huu hana ivo vitu na hawezi kuvipata kwa muda huu.

huo ndio ukweli wa hali zao na wanajua lakini watafanyaje sasa na wakati ukweli unawaambia HAKUNA NAMNA ukiiba utapigwa, ukiomba utanyimwa au utapewa masharti ambayo huyawezi huo ndio ukweli ambao maskini huwezi kuubadili kwa muda huu! ukweli bado unakutaka usubiri, naukweli zaidi ni kuwa unaweza ukaja ukapata au usipate ukafa na ndoto zako! kwani ni makaburi mangapi tumeyazika yamesheheni ndoto ambazo hazikuwahi kufanyakazi duniani.

HUU NDIO UKWELI AMBAO HAUFICHIKI!

Mwengine anayekutana na ukweli muda huu ni

3: Mtu anayekufa, huyu kwa muda huu anajua kabisa kuwa hana chake duniani anaacha kila kitu na hakuna namna yakuendelea kuishi hata kwa dakika kumi zijazo.

masikini ukweli kuwa ndio anakufa muda huu hawezi kuubadili, niukweli unaomuumiza lakini utashi wake hauna mabavu yakupinga.

nafikiri mifano hiyo inatosha.

Shughulisha akili yako ugundue mengine mengi ya ukweli yaliyo ndani yako na ambayo kwa jinsi yalivyo machungu huwezi hata kumwambia jirani yako, rafiki au ndugu.

tambua kuwa wapo watu wanaoficha ukweli kuwahusu kama vile WACHAWI, WASALITI, WANAFIKI N.k nahawa ndio mabingwa wa kuonesha huruma, tabasamu la uongo na upendo wa kughushi.

laana iwe juu yao watu hawa! ni wauaji wa kimyakimya tena ndio haswaa wale mazimwi wenye kukujua, hawakuli wakakumamiliza!

Mungu awashushie gharika, ukweli uwaumbue kabla ya vifo vyao!.

lakini hivi umeshajiuliza utaiweka wapi sura yako siku ukweli kukuhusu ukiamua kujidhihirisha wenyewe mbele ya unaowaficha.

tambua kuwa Ukweli ni kama mbegu unaweza kuificha kwa kuchimba shimo refu ardhini na miaka mingi ikapita mbegu hiyo ikachipua na ikazaa matunda yenye kukufedhehesha wewe uliyeificha lakini kuwanufaisha wale uliowafichia ambao maskini ya mungu huenda kipindi hicho wanakaribia kufa kwa kukosa lishe ya mbegu hiyo uliyoificha na ilikuwa ni halali yao.

Ukweli haufichiki Rafiki, kujaribu kuzuia na kuuficha ukweli ni mithili ya kuzuia mafuriko kwa viganja vyako viwili.

Hakuna Muongo ambaye hajawahi kuitwa mara ya pili kufafanua jambo alilowahi kulielezea huko nyuma.

hii ikiwa ni dalili ya kwamba Uongo mara zote una ulakini na maswali mengi yasiyo na majibu kwa wadadisi.

Mkweli ni mara chache sana kuulizwa jambo ambalo alishawahi kulizungumzia huko nyuma.

Hii ikiwa namaana ya kwamba ukweli una tabia yakujibu maswali yote ya anayedadisi vitu kwa kina hivyo anakosa haja yakumuita mtu kumuuliza labda tu kama anataka kujiridhisha zaidi.

na ubora wa ukweli ni kwamba mkweli akija ataeleza vitu sawa na alivyoeleza mwanzo kwasababu kila kitu kipo wazi na kina ushahidi.

udhaifu wa uongo nikwamba ukimuita mtu aeleze tena maelezo yake lazima ubabaishaji utakuwa mwingi na maelezo yatakuwa na kajiutofauti kidogo na yale ya mwanzo.

Mtafakari kwa kina mtu aliyekufundisha kusema ukweli kisha muone kuwa ni mwenye haki yakutukuzwa.

kwangu mimi ni MUNGU kwenye vitabu vyake ndio amesisitiza ukweli.

yeye ndiye mwenye haki na ndio maana ukweli unapoamua kudhihirika hakuna duniani mwenye uwezo wakuupinga.

mtafakari muovu anayekushawishi useme uongo kisha ona njia yake ilivyo fupi hana mwisho mzuri kamwe zaidi ya aibu nakudhalilika mbeleya uliowaficha ukweli kwa sababu ya maslahi yako au chuki zako.

kwangu mimi shetani pekee ndio bingwa wakuhadaa nakuongopa na kufanya wengine waongope pia.

muone uongo wake ulivyotuponza mpaka kushushwa huku tutafute kwa jasho na wenzetu wazae kwa uchungu.

Tafakari sasa ninani anayekutawala duniani kwasasa MUNGU au SHETANI?

kwa mimi naona wengi sasa mtawala wao ni shetani sababu dunia imepambwa na vazi la uongo lenye taswira ya ukweli.

kwasasa uongo ndio mali, utajiri na kila kitu chenye mvuto.

ukweli maafa, chuki, umasikini na kila kitu chenye kuumiza.

kitu pekee kinachonifariji nikwamba ukweli hauna sifa yakufichwa labda upende tu wenyewe au watu waamue kutofatilia kwa kuridhishwa na ukweli wa kughushi.

nafirijika pia ninapobaini nakuamini kuwa haitafika tamati hii dunia bila UKWELI kubainika.
itakuwa ni siku ambayo waongo watakuwa wamechelewa na wakweli watafarijika kwa kusimamia ukweli wao.

Somo langu kwako leo hii ni hili:

Ukiona kitu chochote kinawavutia wengine wengi nakukitukuza kwa kukifanya ni sehemu ya maisha yao basi rudi nyuma ukitafakati kwa kina kitu hicho.

tafakari kwa kuzingatia mambo yafuatayo
kwanza ni dunia hii ndio ambayo wengi ni wafuasi wa shetani wachache sana wenye imani ya MUNGU.

pili vitu vya kuvutia ambavyo huleta furaha kwenye dunia hii vingi hutokana na dhulma, udanganyifu na niukweli kwamba wanaosimamia haki wanapingwa vikali na ni watu wahali ya chini kabisa yaani madhalili wakutupwa.

sasa chaguo ni lako uishi kifalme duniani kwa kutangaza uadui mbele ya muumba wako au uishi kama dhalili duniani kwa kusimamia maagizo namafundisho ya Mungu wako.

SHETANI AMESHIKA MPINI WA KISU KILICHO FAKE LAKINI MUNGU AMESHIKA MPINI WA KISU KIKALI NA CHENYE KUKATA!

CHAGUO NI LAKO NANI WAKUMSIHI ASIKUKATE.

Utasadiki tu siku moja!
Na
Omar Zongo

Dear Septemba....

 "Mwezi ambao nimezaliwa mimi, Mwezi ambao nauthamini, sijui kwanini hua unakuja nakuondoka mwezi huu, September"

 Na.
Omar Zongo
 
Unaelekea wapi mpendwa!?

iweje unishushe hapa duniani kisha uniache kama hunijui!

ninani mwenyeji wangu!?

inamaana lengo lako nikunileta kisha unitelekeze!!

Jibu lako la jana usiku wakati ukifungusha nguo zako bado nalifikiria eti "nitakomazwa na octoba, novemba na december"

hivi mie nawajulia wapi watu hao! niwewe ndio umenileta hapa duniani niwewe ndio nimekuandika kwenye historia!

niwewe ndio nakufahamu bosi wangu kwanini lakini unanifanyia hivi!!

basi ungeniambia mapema kuwa lengo lako nikunishusha tu duniani halafu utaniacha!
ndio

ungeniambia namimi nikajiandaa kisaikolojia!

nani atanidekeza kama wewe! nani atajua kuwa nimezaliwa katika moja ya siku zako!
ninani atajua kuwa nina vinasaba vya baraka zako!

hujisikii vibaya labda siku ile unanishusha duniani watu walishangilia kila mmoja akisema "Wakiume kazaliwa" wengine wakiandika kifupi kwenye mitandao yao neno HBD.

neno ambalo lilinifariji mno maana wapo waliosema kuwa kirefu chake ni HAPPY BIRTH DAY..

leo unanishangaza mpendwa yaani unaondoka huku ukinifumbulia fumbo la neno hilo eti maana yake HAKUNA BINAADAMU DUNIANI.

Dear septemba kwanini lakini unaniacha wakati kumbe unalijua hilo kuwa hawapo binaadamu nakwanini umewaacha wanifumbie maneno yao ya mafumbo.

bado nahitaji unikuze kifikra usiondoke septemba! unakuwaje radhi kuniacha uyatimani mwenzako!!
Tafadhali septemba usiondoke bwana hebu niambie ninani nitamdekea kama wewe.

Angalau wewe ndio uliwapa nafasi watu wanipendao waeleze hisia zao kwangu!
wengi walileta dua na maombi ya kutimia kwa ndoto zangu.

Unaniacha!?

unaenda wapi lakini! kwanini usibaki namimi unaniachaje kwenye dunia ya dhiki namna hii!
majaribu yakuzidi! fitina mpaka pomoni! uchawi na mikosi! dhiki na ufukara huku raha ikimezwa na shida za aina mbalimbali.

hakika septemba ulioufanya kwangu ni ukatili kunihadaa nami nikahadaika ukanishusha duniani huku wewe ukiendelea.

ahadi yako yakuwa utarudi tena nimeielewa ila tambua kuwa wewe sio mpangaji hivyo sema 'Ishaallah'.

nisalimie uendako maana sina namna yoyote yakukuzuia!

Sitakwambia kwaheri maana neno hilo huua kabisa tamaa yakukutana tena.

Gud bye....
Dear Sept.....
Wako
Mr.Experience

chuki shairi

chuki imekuwa vazi,
 limewakaa mwilini.
kulivua kwao kazi,
haling'oki mauongoni
kama dunia twapita
chuki ya kazi gani.

imewakaa mwilini
imetuwama nyoyoni.
yajionyesha machoni,
imegeuka miwani.
kama dunia twapita
chuki ya kazi gani.

chuki pini nyembamba
yapenya kotekote
si baba wala mjomba
atakuchuki yoyote
kama dunia twapita
chuki ya kazi gani

chuki ikikuhadaa
pigana kuiambaa
ni jumba la karaha
sio kiti chakukaa
kama dunia twapita
chuki ya kazi gani.

chuki ina hila zote
haingojei sababu
ikukuzidia kete
itakuvaa taabu
hii dunia twapita
chuki ya kazi gani

dunia hii twapita
hatutaishi dawamu
litakufika gharika
chuki haina nidhamu
swali nakuswalika
chuki ya kazi gani

ulimwengu una adha
njiaze kadha wakadha
itakupata bughudha
fakiri wakujifunza
kama dunia twapita
chuki ya kazi gani.

SHAIRI: JAWA

"Ni baada tu ya rafiki yangu fulani wakati nipo chuo kuniomba nimuandikie utenzi kumuhusu, kila siku nilikuwa namuahidi nitamuandikia ila siku moja abra ikanishukia na tenzi nikamtungia...."

Na.
BIN ZONGO

Jawa
Malkia
Zawadiwa
Jaaliwa

Jawa
Tunukiwa
pendelewa
Zidishiwa

Jawa kwani nani
mtu gani, ana nini?
jawa mwenye hadhi
sio mpuzi ni azizi

roho yake nyeupe
theluji mithili yake
sema nini akupe
kilicho uwezo kwake

haiba ni vazi lake
stara jaala yake
ucheshi sifa yake
maringo hayapo kwake

Wa UBAVU WAKO

Wazungu wanamuita  soulmate

je unamjua mtu huyu? umeshakutana nae? unadhani yuko wapi??

anza sasa kumfikiria wa ubavu wako maana ni muhimu sana mtu huyu!

kama umempata hewallah laa kama bado fanya hima umtafute mashariki na magharibi usiache akaendelee kuteseka nawe kuteseka kwa nyinyi watu kuishi mbalimbali.

huyo ndiyo sahihi kwako, katika mahusiano yako ya urafiki, mapenzi mpaka ndoa.
yeye ni muendelezo wa akili zako zinapogota kufikiri! yeye ni msaada wa dhati unapokwama katika hali yoyote!

yeye nifaraja unapotokwa na machozi!

amini nakwambia ni mtu aaziz sana huyu.

hatoruhusu ulie! udhoofishwe na mawazo mabaya na ujihisi mpweke.

atakufanya useme "kwanini sikumpata tangu mwanzo mtu huyu!"

hata ujinga wake utakuwa ni burudani kwako!
yote sababu ni ubavu wako umetokana na yeye
wanaoamini uumbaji wa Adam na hawa watasadiki hili

kwanini uendelee kuteseka na mtu ambaye hamuendani? kwako wewe moja jumlisha moja ni mbili kwake yeye ni kumi na moja.

kwanini unalazimishs mtu ambaye hamrandani kimtazamo eti! kwanini unajisahau na unasahau kuwa yupo mwenza wako, wa ubavu wako na ambaye ni sahihi kwako.

sikia, sio rahisi kumpata waubavu wako!

ndio, sio rahisi hata kidogo.

sababu Mungu alipokuumba nakisha kumuumba aliwaamrisha mje duniani lakini sio pamoja amewaamrisha kila mmoja aje kwa mtindo wake.

huenda we umezaliwa Dar es salsam halafu waubavu wako amezaliwa Magila huko muheza Tanga ndanindani.

ila kwasasa yupo kikazi muhinduro!

bado hamjakutana!! wala hamna dalili, na huenda msikiutane!
usipokuwa makini.

usilisahau hili, lizingatie na uongeze umakini katika maombi ili ukutane na waubavu wako.

acha nikukumbushe! baba etu Adam na Mama etu Hawa! walipoamrishwa kushuka hapa duniani nao pia walitenganishwa na ilimchukua muda mwingi Adam kutembea akimtafuta Hawa.

hatimaye akampata!

ilikuwa ni siku ya furaha mno kwa wawili hawa kukutana!

Hapa tena naomba nikumbushe vitu muhimu ambavyo ni asili ya mwanamke ingawa kwasasa vinapuuzwa!
kwanza Umeona hapo juu Adam ndio alihustle kumtafuta Hawa! huezi amini Hawa yeye ivyoshushwa akatulia tuli mahala aliposhushwa hakujishughulisha kamwe kumtafuta mwenzie.

Dah wanawake Mungu anawaona!

Pili siku ambayo Adam anamuona Hawa baada yakutembea maili nyingi kuchomwa na miba, kukimbia wanyama wakali na dhoruba kadha wa kadha Huezi amini Hawa alikuwa anajificha kwa aibu.

wala hakufanya maigizo ya "waooh jamani tumeonana tena! nimekumis wewe!!"

No, hajafanya hivyo kabisa..! ndio kwanza alikuwa anajificha ficha kwa aibu na niyeye ndiye wakwanza kumuona Adam lakini hakumshtua kabisa kwa aibu mpaka Mzeebaba alipomuona mwenyewe.

Aibu ni asili ya mwanamke na sio uchakaramu wakuropoka hovyo kama umekunywa maji ya chooni.
mxxxxiiiieee!

Turudi kwenye mada! tambua kuwa waubavu wako yupo!

somo hili limewapita watu kushoto ndio maana maumivu ya mapenzi kwasasa mengi mno.
yamejaa pomoni!

maumivu lazima yawepo sababu watu wanachukuana chukuana tu bila kujua kuwa unayemchukua sio aliyotokana na ubavu wako.

sasa unadhani asikuumize kwakuwa wewe nani!

atakuumiza tu! na tena mie nasema uumizwe tu maana hakuna namna sasa.

ni lazima akuumize sababu haoni uchungu wowote maana wewe sio wake kwa hivyo nafsi yake haimsuti hata kidogo kukutenda.

ni tofauti na waubavu wako! yeye akikuumiza hata kwa bahati mbaya atajutia kosa hilo na litamuumiza sana kama vile ameumizwa yeye.

ina raha ukimpata mwenza wako! acha tu yani...

ukilia atalia na wewe hata kama hajui kinachokuliza!
tatizo lako litamgusa kama vile lakwake

kiukweli ni somo pana hili kuhusu waubavu wako na kwa vipi utamjua kama huyu ndiye.
kwakweli inahitaji umakini sana maana sasa wamejaa wengi kila mmoja akijifanya ndiye yule wa ubavu wako.

ndiyo! wengi huweza kuja kwako wakiwa wamesheheni sifa lukuki za waubavu wako.
nina uhakika laiti kama wangelijua jina lake basi WANGEKUJA KWA JINA LAKE! pia.

tena huigiza nakujikuta wakizidisha mbwembwe za mambo mazuri kua
shinda hata waubavu wako!

hawa wapo na kwasasa wamezidi ulimwenguni!
utawajuaje!?

hili ni swali zuri najibu lake ni ngumu kuwajua hivyo umakini unahitajika na kusubiri huku ukimuomba MUNGU ni njia iliyo sahihi zaidi.

acha tamaa ya gari zuri, pesa na maisha mazuri!

huenda siku moja waubavu wako akaja na vitu hivyo!

au vitafute kwa njia nzuri ya halali ili siku moja uvitumie ukiwa na wa ubavu wako.

maana athari zakuhadaika na waubavu wako wauongo ni nyingi nitakutajia chache.

kwanza hatakuthamini kutoka moyoni bali ataigiza tena zaidi akiwa mbele ya macho yako tu, ukiondoka atakung'ong'a nakukupuuza.

atakuwa tayari kufanya lolote zuri ili aendelee kukutumia, kukuchezea nakukunyonya vyote anavyovitamani kutoka kwako,

amini au usiamini ukipatwa natatizo kubwa utalia na ndugu zako yeye hataguswa, abadan.
pia mazuri yake yana mwisho yaani inafika kipindi hafanyi tena aliyokuwa anayafanya mwanzo mazuri yaliyokuwa yanakuvutia.

na hiyo ni tofauti na waubavu wako! kamwe narudia tena kamwe hawezi kuacha kusimamia furaha yako.
hata asiposema lakini vitendo utaviona na vitakudhihirishia kuwa yeye kwako ni Washida na raha, shibe na njaa, uzima na maradhi umasikini na utajiri.

Fumba macho umuombee waubavu wako popote alipo asogee karibu yako akutoe mikononi mwa walaghai.
pia asiendelee kutumiwa na watu ambao sio wake.

ni mahusiano machache sana duniani yamekamilishwa na wawili ambao wameumbwa wawe wao
na utawagundua kwa historia zao, itikadi zao na namna ambavyo walivyo tu utawagundua na utawafurahia!
watakuvutia!