mtandaoni shairi

 Na
Bin Zongo

karibu mtandaoni
uyaone ya duniani
karibu keti makini
ujue nani ana nini

bando la uhakika
bando halina shaka
insta kunafikika
twitter nakadhalika

simu yangu smart
tabu tabu sipati
maridadi internet
karibuni tuchart

naanza nae Kimambi
Mage haeshi vitimbi
leo kapost mengi
post zake hupingi

alaani serikali
ina nyingi dosari
viongozi dhoflehali
insta kote zohari

mateja wazodolewa
polisi wanatakiwa
mkuu kashaamua
mkoa kusimamia

apost vita vyaanza
biashara
tokomeza
harakati ndo imeanza
madawa kuyamaliza

wengine niwapinzani
wameanzisha tafrani
eti mkuu hajulikani
amesoma shule gani

mengi ya mtandaoni
hufurahisha moyoni
eti mchungaji gani
amezaa kwa kuzini

yule na wimbo mpya
huyu na demu mpya
mondi kaibua jipya
bifu limeanza upya

PANDE MBILI ZAZOZANA

Pande moja imevaa gauni ishara ya mwanamke nyengine imetinga kanzu ishara ya mwanaume!
moja ya kanzu yasema wake waharibifu uaminifu hawana wamejawa mapungufu.

gauni lataharuki almanusura livuke lasema hayasadiki waume wanachosema wao ndio mamruki uaminifu hawana.

kanzu yatetemeka mate kinywani yatoka maneno yaropoka waume wametukuka, wanawake kwa vibweka duniani wasifika.

Gauni latabasamu kwa dharau na kiburi lasema huna nidhamu mwanaume baradhuli ukishaishiwa hamu mwanamke humjali
hauna ubinadamu wanaume ni zohari.

Kanzu yakunja ndita mijicho yachomoka, kukupiga sitosita hivi ndivyo yaropoka
sema nami kwa nukta dharau sitazitaka.

Mwanamke gauni asema sikuogopi sitoshuka chini maneno yangu silipi
tena yana thamani wanaume ni makapi.

kanzu yagadhibika busara yamtoka matusi aropoka gauni lamcheka.

Bi Gauni : tukana utukanavyo ila habari unayo, hivyo ndvyo mlivyo waume mapoyoyo, hasira zenye ujazo ni mapungufu hayo.

Bwana Kanzu : wanitafutia kesi mwanamke hayawani nyinyi bidhaa nyepesi twawaona mtaani siku izi mna kasi sio kama wazamani.

Bi Gauni : sisi ni mama zako tazama mdomo wako huo udume wako ukome matusi yako zungumza kwa staha nione udume wako.

maneno hayo mkuki yamchoma bwana kanzu ukweli haukwepeki umemvua kwa nyavu.

Bwana Kanzu : nisamehewe kwa hilo mie kanzu kweli juha lakini mnapotea kutanga tanga najua waja msotulia gauni nakuambia.

Bi Gauni : ninyi apo ndio chanzo chasisi kuhangaika, mmetufanya chotezo nyie maji mwamwagika mbinu zenu hamnazo kulaghai mwasifika.

Bwana Kanzu : tatizo uaminifu ndio kitu mnakosa waume walinganifu hatujaiga usasa
usagaji maradufu
eti mambo yakisasa.
hamnayo tena hofu
kujibadili kabisa.

Bi Gauni : ushoga nao wanani waume mwaaibisha
hayakuwepo zamani
mambo haya kabisa
aibu hebu oneni dunia itawakosa
marijali hatiani
wamejaa wakibisa.

Bwana Kanzu : umenionya matusi sasa mbona watukana mwanamke wewe nuksi tafsida hata huna
utakupata mkosi baba akikupa lana.


Bi Gauni : ukweli unaumiza mithili ya tusi kuu
nikweli nakueleza
wanaume mpo juu
tamaa zinawaponza
kutaka mambo ya juu.


Bwana Kanzu : midomo yenu jeuri ndio mana hatuwaoi
kimewajaa kiburi tunawatoa nishai
maisha yenu dhalili
acheni kujidai.

Bi Gauni : kuolewa kazi gani waoaji siwaoni wasasa ni matufani simuoni wathamani
mwanamke pambo ndani ataka mtu makini.

Bwana Kanzu : siwezi bishana nawe waweza nipa kesi bora niachane nawe hoja zako nyepesi.

Bi Gauni : toa zakwako nzito mwanaume huna haya mmegeuka watoto siku izi twawalea mambo yenu mpito mmezidisha mabaya.

Bwana Kanzu : nanyinyi hamjioni mavazi yenu dhalili.
mwakatiza mtaani
utupu juu ya mwili
tena hatuwatamani
kwasasa hamna dili

Bi Gauni : nacheka cheko la haja mwanaume hujijui tumeumbwa kwa lahaja nzuri huitambui tena andiko likaja kujiremba tanabai.

Bwana Kanzu : urembo gani ujinga utupu wenu thamani
urembo huo napinga
haupo maandikoni mwanamke we mjinga kutetea ushetani.


Bi Gauni : tumeumbwa tofauti usituhukumu wote
mwanamke humkuti
kaacha maungo yote
hao uwasemao sio wanaake wote.


Bwana Kanzu : kumbe walijua hilo sasa porojo zanini
hata sisi nasi pia tumeumbwa kwa makini wapo tulotunukiwa urijali mauongoni na wapo waliopewa ukike kike fulani.

Bi Gauni : basi kama hivyo ndivyo lawama weka pembeni sote tumeumbwa hivyo tofauti ni kichwani!
tuache habari hizo nakuhitaji chumbani nataka muendelezo
wa hoja tukiwa ndani....

Gauni latabasamu huku likijisemea "wanaume bwana yakwao ni haya tu haya hoja gani za chumbani.....hahahaaa makubwa haya acha nikamsikilize...!"

Na
Omar Zongo
SIMULIZI ZINAISHI