Nini kifanye nisikuheshimu rafiki, Naahidi ntakuheshimu sana sio eti sababu ya pesa zako, au cheo chako au labda sababu sjui umenizidi au nimekuzidi nini, au pia usije dhani ntakuheshimu sababu kuna kitu nataka kwako au mimi ni dhalili LA hasha!!, sitakuheshimu kwa sababu hata moja hapo juu, ntakuheshimu sababu HESHIMA Nimefunzwa, na nikaambiwa utu wema huundwa na HESHIMA.

Hakika nakwambia kamwe sitaacha kukupa heshima yangu ilojaa pomoni!
Lakini rafiki naomba unielewe HESHIMA yangu haitamaanisha kuwa NTAKUOGOPA,
Woga ni kitu kingine kabisa ambacho siamini kama kinaishi ndani yangu!.
Acha nikupe story kidogo:
Mara zote
upendo uliongezeka kutoka kwa Mzazi wangu pale nilipoonesha namuheshimu sana na sjui kwann lakini alinichukia sana alipokua akigundua Nina kawoga fulani juu yake na wakati mwengine aliniambia SIPENDI MTOTO MUOGA!.
hakika rafiki sitakuogopa ila kwa dhati ya moyo wangu naahidi nitakuheshimu kadiri niwezavyo...
utapata shida bure kunionesha nguvu zako,majigambo, uwezo na sjui nini ulichonizidi ili nikuogope, sana sana nitakunyima vyote na hata heshima yenyewe sitakupa, nitakudharau na sitakuogopa halafu utaona kuwa wewe ni sawa na mzigo wa kinyesi nimekuvumilia kwa uzito umenishinda kwa harufu! Ahahahaaa ntakuheshimu rafiki sitakuogopa milele!