JUNIOR

 "Sikuwahi kusimulia kisa cha kweli nikakiruhusu kusomwa na watu pengine hii inaweza kuwa simulizi yangu ya kwanza yenye ukweli ndani yake, ni zawadi kwa ndugu yangu Ramadhan Madebe ambaye kwa asilimia kubwa amechangia ukamilifu wa simulizi hii....ni sehemu ndogo pekee ndio yakubuni lakini mengi yana ukweli....."

JUNIOR

SEHEMU YA KWANZA

Niliona wivu sana baada ya rafiki yangu kupewa jina na dada yako, yeye aliitwa mwinjuma lakini alimbeza jina lake hilo na akasema kuwa anapendeza zaidi akiitwa Geminus!

Leo ndio nagundua kuwa aina ya familia bora kama ilivyo ya kwenu ndiyo huwaaribu watoto nakuwafanya wayachukie majina ya Kiswahili kutokana na wao kukesha wakitazama filamu za kizungu na kihispania.
Hata kama muhusika mkuu katika filamu ya kizungu akitokea anaitwa Zongo, mradi ni mzungu na anacheza vizuri kwenye nafasi yake basi jina hilo linaweza kuwa ni jina zuri kuliko yote duniani.

Kiukweli licha ya kuwa akili yangu ndogo lakini imebaini kuwa hili ni tatizo ingawa nakiri sina utaalamu wa kutatua tatizo hilo maana ni tatizo kubwa linalohusu saikolojia zetu waafrika.
Nakumbuka Rafiki yangu Mwinjuma alivyobadilika jina nakuitwa Geminus nilikuja kwenu bila haya nikakulalamikia nikakwambia namimi unitafutie jina.

Sauti ya jibu lako bado inajirudia kichwani mwangu “usijali, acha leo nikeshe nikiomba naamini kesho nitakuja na jina zurii ambalo litakufaa”
Hivi ndivyo ulinijibu, nakumbuka nilifarijika sana na nikarudi nyumbani kwetu kwa furaha nikiiomba kesho ifike nilisikie jina langu ambalo umenichagulia wewe.

Sikujali kuwa mimi nimekupita umri na wewe ni makamo ya mdogo wangu, hilo sikulijali kabisa niliona na kukiri kuwa umenizidi upeo.

Sikujali pia umbali wa kila siku kutoka kwetu uswahilini kuja maneneo ya kwenu uzunguni ambapo hii ni kawaida kwa nchi zetu za kiafrika mitaa kujitenga kutokana na vipato vya watu wake.
Nina uhakika kama familia yako ingekuwa na kiburi kutokana na neema ya utajiri basi mimi na rafiki zangu tusingeweza kabisa kukanyaga nyumbani kwenu lakini nashukuru sana na kila siku nauota ukarimu wa wazazi wako, na ucheshi wa ndugu zako.

Nakiri kuwa hii ni historia ya miaka mingi sana ya nyuma lakini bado inaishi kichwani mwangu zaidi siku hii ambayo uliviweka viganja vya mikono yako usoni mwangu.
Ulitaka kuhakikisha kuwa nimeyafumba macho yangu yaani sioni kitu, uliniambia hilo ndilo sharti la wewe kunitajia jina langu jipya ulililonichagulia.

“kuanzia leo utaitwa Junior” hii ni sauti yako ambayo naisikia mpa
ka leo ikitamka maneno hayo, tangu hapo namimi nikajivunia kuitwa Junior.

JUNIOR
SEHEMU YA PILI


Yote hayo yalikuwa yanajiri tukiwa shule ya msingi, mimi nikiwa nimekupita madarasa matatu, sijui kizazi chetu kimekumbwa na nini masikini yaani tunayajua mapenzi tangu tukiwa wadogo.

Ndio maana mpaka leo muda huu unasoma ujumbe wangu bado mwenzako nastaajabu na hila za mapenzi, ukweli ni kwamba kati yetu kulikuwa na upendo! Lakini utoto wetu ulikuwa chanzo cha sisi kushindwa kuelezana ya kwamba tunapendana tena sio kimasikhara yaani tunapendana sana.

Zaidi tuliishia kucheza pamoja huku kila mmoja akifurahia ukaribu wa mwenzake, kwangu mimi ilikuwa siku mbaya sana ikiisha bila kuiona sura yako sijui kwa upande wako.

Mdogo wangu ambaye ulikuwa unasoma nae darasa moja sijui kwanini alikuwa ananificha kuwa mkiwa pamoja hua unanisifia nakumwambia kuwa mimi ni mstaarabu sana, ndio! mimi ni msataarabu na sijui kwanini nilikuacha mwanamke ambaye uligundua ustaarabu wangu tangu nikiwa mdogo.

Nakumbuka zama zile na natamani zijirudie angalau niwe karibu nawe nikiwa na akili za sasa hivi ili nikwambie neno nililostahili kukwambia kipindi kile nikashindwa.
Ujinga wa utoto ulinifanya nikahadaika na binti mwengine ambaye aliibua wivu wako wa kitoto na ukaanza kujifunza kunichukia tangu hapo.

mwisho wakuiona sura yako ilikuwa ni mimi wakati namaliza kidato cha nne, maisha yalitutenga nakutuwekea mpaka mkubwa uliofanya hadi hii leo sura yako ibaki kuwa kumbukumbu tu.
Asante teknolojia walau sasa nakuona mtandaoni.

Sikuamini kabisa kuwa ungenijibu ujumbe wangu mfupi nilipokusalimia kwa mara ya kwanza Facebook, sikuamini pia uliponijibu kuwa ni wewe ndiye Yule mwanamke wangu wa kwanza kuvutiwa nae duniani hapa.
Ujio wako umekuja siku chache tu baada ya maombi yangu kwa mungu pamoja nakufunga ili anioneshee mke mwema. Sababu nataka kuoa mwenzako.

Kukutana tena kwa mara ya pili nawewe imekuwa ni faraja kwangu nikiamini kuwa umeletwa na Mungu.
Kauli yako ya jana ndio imenitoa kabisa kwenye imani yangu! Siamini kabisa kama ni kweli umeolewa na una watoto wawili.

Masikini mimi nilikuwa wapi! Kwanini sikuwahi kujua kuwa ni wewe ndio nilipaswa nikung’ang’anie.
Unasema hauishi kwa amani na mume wako, ni Malaya na hana kabisa upendo. Amekulaghai kwa pesa zake na sasa haioni thamani yako tena.

Ilikuchukua mud asana kunielezea haya, ulikuwa hutaki kwa sababu ya kuficha maovu ya baba watoto wako, lakini nilipokubembeleza sana ndipo siku moja ukanidokeza japo si kwa undani.
Uliniumiza zaidi uliponiambia kuwa jamaa hakupi haki yako ya ndoa,licha ya kuwa unambembeleza sana.
nafsi yangu ni nzito kukwambia utoroke uje maana najua watoto wako wanapaswa kupata haki ya kulelewa na baba na mama yao.
Naogopa kesho huenda wakanihukumu kuwa nilikuachanisha na baba yao, naogopa pia dhambi maana imani yenu haiwaruhusu kuachana kamwe na mnahitajika mpendane kwenye shida na raha kama mlivyoapa siku ile mnafunga ndoa kanisani.

Lakini kwanini urudi wewe mawazoni baada ya kumuomba Mungu anipe mke mwema! Tafadhali nijibu kama ukipatwa na fahamu maana nimeambiwa na rafiki yako kuwa mume wako amekupiga sana juzi na hivi sasa upo chumba cha wagonjwa mahututi, hali yako ni yakuombewa! Maana humjui aingiaye wala atokaye.
Kwanini wanaume tuko hivi, amewezaje kuutendea maovu mti mbichi namna hii au nikwasababu haijui asili yako,
Nakumbuka kuna siku ulizungumza na baba yangu kwenye simu, mzee wangu ni mtaalamu sana wakugundua tabia ya mtu hata kupitia simu, na nilisubiria maoni yake baada ya kuongea nawewe, sikuongopei alikusifia sana na ajabu alipokutaja kwa mama ndio sifa nzuri juu yako zikazidi, wadogo zangu bado wanakumbuka zawadi na upendo wako kwao, kwa mfano mdogo angu Naa mpaka leo kuna gauni lake ulilomzawadia amelitunza sana licha ya kuwa limemruka na halivai tena lakini anasema ni kumbukumbu ya mdada mkarimu aliyewahi kumjua maishani mwake.

Kiukweli najikaza tu nisilie hasa wazazi wangu wanaponiuliza habari zako ninapoenda kuwatembelea, nashindwa kuwaambia kuwa nilikupoteza.

Sasa nafahamu kuwa kweli mimi ni JUNIOR! Ulikuwa mkubwa kwangu kiupeo na ulijua thamani ya upendo licha ya kuwa umri nilikuzidi na ndio maana uliniambia kuwa “huezi kuendelea kuwa namimi maana nimesoma na wewe unahitaji kusoma” aya maneno yako yalikuja baada yakugundua kuwa mimi nina mwanamke mwengine.

Naomba upone haraka unisaidie kunijibia maswali yangu nini nifanye maana niwewe ndiye nimeonyeshewa baada ya kumuomba mungu lakini ni wewe ndiye ambaye kwa sasa ni mke wamtu.
Tafadhali amka Anna kwa sasa mimi sio Junior Tena mtaani wananiita MR experience, nina uzoefu mkubwa na haya maisha na ninajua pia thamani ya upendo.

Plz Anna amka, nipo na wanao hapa Mumeo amesafiri mchana huu kikazi, ndivyo alivyodai wakati amepigiwa simu kuelezewa hali yako lakini kwenye mtandao wake wa kijamii namuona amepost yuko hoteli flani Arusha na mwanadada mrembo lakini hakuzidi wewe Anna,
Plz naomba uamke unipe dira yangu Katika mapenzi…nahitaji kuoa mwenzako.
Na
Omar Zongo

Inaendelea….
SEHEMU YA TATU

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »