WARAKA WA JPM

 Huu ni waraka wa kufikirika wa Hayati John Pombe Magufuli, Rais awamu ya tano wa Tanzania ambaye alifariki dunia usiku wa tarehe 17 march mwaka 2021...


Muandishi wa waraka huu ni Omar Zongo

Kutokea Eneo ambalo wanaenda waliokufa tumepokea waraka huu.

Waraka wa JPM.

Anasema....

Ndugu zangu watanzania,    ile siku ambayo roho yangu iliusaliti mwili wangu, ilikuwa ndio siku ya kwanza ya mimi na ninyi kutenganishwa katika ulimwengu huu wa Roho na Mwili.

Sikuwa na namna yoyote ya kupinga rungu la malaika mtoa roho, ninachoshukuru ni kwamba udongo umeudhibiti mwili wangu lakini Roho yangu ingali hai hata kupata uwezo wa kuyaona yanayoendelea Duniani, lakini zaidi kuwaandikia waraka huu.

Nimelazimika kuuandika waraka huu kwa sababu nyingi lakini kubwa ni hili tendo linalotarajiwa kujiri hivi karibuni 

Tendo la kuuaga mwaka uliogharimu maisha yangu.

Najua nimesaliti kiapo cha Uongozi, kwa kuwaacha kabla ya muda, lakini ningewezaje kupinga mapenzi yake Mungu.

Katika waraka wangu huu wa leo sitaongelea kwa kukosoa hata kimoja kuhusu uongozi wa Samia Suluhu kwa sababu kila nabii na zama zake hivyo, KAZI NA IENDELEE.

Kama nyani mzee tu nilikwepa mishale mingi enzi niko hai lakini ule mshale ulionitandika ndani ya mwezi wa tatu wa mwaka 2021 sikuweza kabisa kuukwepa.

Ulikuwa ni mshale wa mauti yangu na hata mbinu zote ningetumia kuukabili isingewezekana abadani.

Hiyo inatokana na kweli wa kwamba sikuwa wa kwanza kunyanga'anywa roho na wala sitakuwa wa mwisho.

kesho yako na wewe inakuja!!

Jiandae!

Kuna nukuu zangu nyingi kwenu zimebaki kama ushuhuda wa kuwa nilijua kuna siku nitakuja mahali nilipo kama ambavyo nafahamu kuwa na wewe utakuja, suala la nani atangulie ni siri ya Mungu.

Sikutaka kutenda hovyo katika wakati wangu ndio maana nilijitahidi sana kuacha alama.

Kama katika juhudi zangu hizo kuna mtu alikwazika basi aruhusu moyo wake usamehe maana maisha ya mwanadamu duniani huambatana na mapungufu yake.

Zile Siku chache baada ya kifo cha mzee mkapa zilikuwa ni siku za maandalizi ya kifo changu.

Balozi kijazi alilazimika kunitangulia ikawa simanzi kwangu hata udhaifu wa afya yangu ukawa maradufu.

Mfululizo wa vifo vya watu wazito waliokuwa chini yangu katika taifa langu ulikuwa ni ishara mbaya kwangu lakini sikupata mfasiri akanipa maana ya mambo yale tanzia yaliyojiri kwa kufuatana.

Maalim Seif niko nae huku, Anna Mghwira niko nae huku Jaji Ramadhami niko nae huku na jambo la kufariji ni kwamba naandika waraka huu ukiwa umepata baraka zao wote watu niliowataja.

Watanzania msiache kumtanguliza Mungu katika kila jambo, vikwazo na majaribu ya Dunia havishindwi na maarifa ya mwanadamu peke yake.

Kesheni mkisali kuliombea Taifa lenu, amani iendelee kudumu na raslimali za nchi yenu ziwanufaishe watu wote.

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere anawasalimia sana huku tulipo tunakesha tukiwaombea mzidi kustawi na kuwa taifa kubwa na lenye nguvu ulimwenguni.

Nitumie nafasi hii kuwatakia heri ya mwaka mpya na kila jema liwafikie ndani ya mwaka 2022.

2021 imeondoka na zigo kubwa ambalo ndani yake ipo roho yangu ila isiwe chanzo cha kuuchukia huo mwaka Mungu apangalo halijawahi kushindwa.

Poleni wafanyabiashara wa kariakoo mlio unguliwa na soko lenu, ujenzi ukikamlika nina imani mtarudi kuchapa kazi.

Kuanguka na kusimama ndio ladha halisi ya maisha ya duniani hivyo miskate tamaa ba hasara iliyojitokeza.

Ndugu zangu machinga kuweni na moyo mkuu na mfuate maagizo ya mamlaka maana mamlaka zote duniani zinawekwa na MUNGU hivyo fuateni utaratibu ili kudumisha mshkamano na amani.

Niwatakie kila la kheri ndugu zangu watanzania msisahau ya kwamba Huu ndio msimu wa kufanya biashara na SIMULIZI ZINAISHI GROUP ni sehemu sahihi ya kubrand biashara yako..

Wasiliana nasi 0788777658

Ili kupata maandishi yetu kwa sauti Usiache kutembelea youtube channel yetu SIMULIZI ZINAISHI kwa kjubofya link hii hapa chini

 https://www.youtube.com/results?search_query=simulizi+zinaishi

Share this

Related Posts

Latest
Previous
Next Post »