MAJIBU YA BARUA YAKO MAKAYULA

''Nimeipata nafasi yakujibu salamu zako ulizoniandikia Makayula. sina shaka utaniambia mbeya wangu ninani"

Na
Bin Zongo

Mpaka kuandika waraka, najua umesalimika
Afya yako sina shaka, nilipo nina uhakika.
taharuki imenifika ,yanigubika mashaka.
ninani mbeya wangu, Makayula nieleze.

Urafiki nishakataa, wanafiki waja waleo
Mabingwa wakuhadaa, sikitaki icho cheo
Waraka nimeshangaa, usemayo yote siyo
ninani mbeya wangu, Makayula nieleze.

Nyumba yangu ipo sawa, amani iko pomoni
Fikira hasi ondowa, zibakishe tu moyoni
Sisikie yakuambiwa, mengine ni ya kubuni
Ninani mbeya wangu, makayula nieleze.

Mie ni yuleyule, watangu tungali shule
Haiba yangu upole, sijayaiga ya wale
Ndoto zangu zilezile, kesho nifikie kule,
Ninani mbeya wangu, Makayula nieleze.

Umechotwa na mtego,umevalishwa hasara
Wamekugeuza zigo, kukupa habari uchwara
Hebu liambae pigo, kwa kusimama imara
Ninani mbeya wangu, Makayula nieleze.

Shemejio ana raha, mie tunda la peponi
Kwake hakuna karaha, furaha yake moyoni,
Usemayo yakuzua, pinga usiyaamini,
Ninani mbeya wangu, makayula nieleze

Majivuno kwangu sumu, alinihusia mama
Tena kitu haramu, kwangu hayajatuwama,
Nimefundishwa nidhamu, vazi langu heshima.
Ninani Mbeya wangu, makayula nieleze.

Kama haya umezua, rafiki chunga ulimi,
Nafsi yangu yaugua, tabia hizi simimi,
Ninani alokwambia, ni ruhusa kujihami,
Namtaka mnafiki wangu, makayula nieleze.

Uchawi ndio kitu gani, dhahania sizijui
Mie kwetu muumini, shiriki sizitambui,
Kwanza mgeni Handeni, Muheza najidai
Ninani Mbeya wangu, makayula nieleze.

Haya maji marefu, kuoga yataka mbavu.
Tena uwe mrefu, kichwani usiwe mkavu,
Kuepuka mapungufu, ujihami nazo nyavu.
Ninani mbeya wangu makayula nieleze.

Mwenzako mie mgema, leo umeiba muda,
Umenitaka kusema, pombe yote mdabwada
Hasara imesimama, ila sawa hamna shida,
Nimtakaye mbeya wangu, makayula nieleze
Na.
BIN ZONGO

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »