This Iz My Sister


Na.
OMAr ZONGo

Hey niaje, naitwa Jayvny, kwetu tumezaliwa wawili tu, mimi na dada 'angu, yeye anaitwa Jackline.

Tumepishana miaka sita mimi nayeye!!, tunapendana sana mimi na dada angu licha ya yakwamba tumetofautiana baba.

Nataka kukupa kitu chakujifunza Leo kutoka kwa dada 'angu.

Sitakwambia amepitia mangapi mpaka kumuita shujaa kwenye Andiko hili ila nitakwambia kuhusu Moyo wake wa chuma.

2014 terehe 01, mwezi wa 11, ndio siku tulimpoteza mama etu, nikiwa Na umri wa miaka 16.

Mama aliondoka ghafla duniani, hakupata hata nafasi yakusema 'kwaherini wanangu'.

Alituacha mimi Na dada 'angu tukiwa wakiwa, tena wapweke wenye donda kubwa la maumivu ya kifo cha mama etu mpendwa.

Nakumbuka kifo cha bimkubwa kilinifanya nilie sana, nilipoteza fahamu.

Nakumbuka nilipozinduka nikajikuta nimelala chumbani, kichwa changu kikiwa juu ya mapaja ya dada.

Nilifumbua macho kuangaza humu ndani, vilio vya chini chini vilisikika kutoka kwa watu wengi waliomo humu.

Niliwatambua,

Wengi walikuwa ndugu zetu.

Ndio, ndugu zetu,

 Walikuwa hapa kuomboleza msiba wa mama 'etu.

Dah!! Akili ilinirudi!!

Masikini mimi nilikuwa kwenye siku za msiba wa mama angu, siku za majonzi makuu!.

"Pole Jayvny" sauti ya dada ilisema.

Niligeuka kumtazama, ni wa ajabu dada angu, alikuwa anatabasamu.

Kwa siku hii kwakweli sikumuelewa, nilidhani hakuwa Na uchungu na kifo cha mama.

Lakini sivyo!!! Ni dada ndio alikuwa ameguswa Na msiba ule pengine kuliko mie niliyezimia.

Ndio!!

dada ndio aliguswa zaidi, maana alijua kuwa majukumu ya mama yooote sasa yalimgeukia yeye.

Ule mkopo wa benki ambao mama aliuchukua ili afungue Biashara iliyovunjwa Na mgambo kisa iko barabarani, sasa ulimngoja yeye.

Kodi ya nyumba tuliopanga ambayo mwenye nyumba siku zake ziliisha zakusubiri, ilikuwa yakwake.

Ada yangu ya shule ya gharama ninayosoma, tayari muhula ulishakaribia kuanza.

Hayo Na mengine mengi sasa yalikuwa yanamngoja da' Jackline.

Lakini kwenye msiba wa mama alikuwa ameniweka mapajani kwake akinifariji nakunisihi ninyamaze kulia!!

Nakumbuka alisema "mama yupo nasi, ataendelea kua nasi, anatupenda na hapendi kuona tukisononeka maana ameenda kupumzika kwa MUNGU aliye hai"

Maskini dada!!

 Sikumuelewa, kumbe alikuwa anasimama imara yeye ili kunifanya kunifariji mimi.

Kumbe alikuwa anasimamia falsafa ya 'magumu hupita'

Hata baada ya mtihani ule, maisha yaliendelea.

Hakuwa Na kazi lakini alihakikisha nyumbani pengo la mama halionekani.

Mara zote alimtaja Kristo akisema ndio kimbilio letu.

Alisema kamwe hatutaanguka tukimtumainia bwana.

Hata aliyempa ujauzito alipokataa kulea mtoto dada hakuacha kujipa sababu zakulea nakumpenda mwanae.

Siku zote alisema maisha ni mazuri sana, alisema kila kitu kinapangwa na Bwana, alisimama imara Na lile tabasamu lake alilonionesha siku ile kwenye msiba wa mama.

Leo hii nakusimulia kuhusu dada angu imepita miezi sita tangu nisimame kwenye kitanda chake, maumivu makali ya maradhi yakiwa yamemdhoofisha.

Nakumbuka siku zile mara zote nilizokuwa nikimuona kitandani amelala hoi, machozi yalikuwa hayaachi kunitoka lakini yeye bado aliendelea kunifariji kwa sauti yake ya uchovu wa maradhi.

Alisema "Jayvny nitapona tu hivi karibuni, kila siku afya yangu Inaendelea kuimarika"

Maneno yake haya alikuwa haachi kuyasema, ingawa ukweli haukuwa huo kabisa.

Kila siku dada alikuwa akizidi kuwa hoi kitandani.

Hata siku ambayo alikutana na daktari wa kiroho, akampa tiba ya matumaini nilishindwa kuamini kama atapona.

Lakini hatimaye kweli dada akapona, afya yake iliporejea akasema "nilikwambia Jayvny, hatupaswi kulia magumu yakitufikia, ni mapito tu, ona sasa niko mzima."

Huyu ndio dada angu ambaye hivi sasa naongea nawewe niko nae kwenye chumba cha mauti.

Tumetekwa Na watu wasiojulikana, watesi wetu hawachoki kutupa adhabu bila sababu ya msingi.

Wanaionea miili yetu kwa vitu vyenye ncha Kali, wanatuadhibu kwa chakula kidogo nakutulazimisha kufanya yaliyo kinyume Na utu wetu.

Mwisho wa maisha yangu nauona, hali ya kukata tamaa imenitawala lakini bado dada angu haachi kusema "MUNGU ameruhusu haya yatufike, ana maana iliyo nzuri wala tusilaumu, endelea kuamini kuwa maisha yetu yabaadae tukitoka hapa ni Bora na mazuri mno"

Nashindwa kumuamini dada maana mateso yametuzidi kwakweli lakini namshangaa uso wake wenye damu kila mahali bado una lile tabasamu lake la faraja..

Anaitwa Jackline,
Ni jasiri, hakati tamaa, mpambanaji Na mwingi wa imani.

THISI IS MY SISTER.
Naamini tutatoka hapa.

To be cont....    


SiMUlizi ZinAishI

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »