Kifo chako kikitokea


Kifo chako kikitokea, kitawashtua wanaokujua Na wengi watakulilia lakini zaidi watakaoumia ni wale walio karibu na wewe!

Pia kwasasa upo hai,Wapo ambao unawakera nakuwaudhi lakini kwa unafki wao siku hiyo watasema kuwa wewe ni mtu mwema sana.

Moja ya fikra zako muda huu upo hai ni labda siku ukifa mzigo wa majukumu yako ataubeba ndugu yako flani, kisa anakuchekea, anawafurahia watoto wako, mke au mume wako.

Labda kisa mnasaidiana sana na ushamtendea mema mengi! Unajifariji huenda yeye atavaa viatu vyako, atawasomesha kwa moyo mmoja, atawaongoza nakuwafariji bila Tatizo.

Sipingi hisia zako inawezekana zipo sahihi, lakini acha nikufikirishe tofauti kidogo!

Tambua kuwa binaadamu tumeumbwa Na unafiki wa asili!

Wengi wao waliokufa walijifariji kama wewe lakini matokeo yake watoto wao wanadhalilika, ni ombaomba Na wengine hawana ndoto tena.

Au wengine walibahatika kulelewa lakini kwa dhiki Na masimango makubwa, makovu ya mateso waliyopitia wanayakumbuka hadi Leo.

Ipo hivyo rafiki yangu, hivyo

Siku ukifa wakati unalilia dhambi Na matendo yako uliyoyafanya usiache kulilia watoto na majukumu yako unayoyaacha.

Lia ukijiuliza ninani atawafariji nakuwatimizia ndoto zao.

Je yupo ambaye utu Na thamani yako ataendelea kuvienzi kwa kuwafariji wanao nakuwafuta machozi daima.

Je yupo ambaye atataja sifa zako kwa wema hata baada ya mwaka mmoja wa kifo chako.

Je yupo ambaye atalipa fadhila kwa kuwatendea wema wanao ambapo Pengine ulikuwa ukifanya wema ili siku moja nao waje watendewe wema.

Naogopa kusema moja kwa moja kwamba siku ukifa itakuaje lakini historia inaonesha wengi walipofariki waliacha mwanya wa familia zao kuonekana takataka Na hata kuwatenga wakati mwengine.

Nachelea kusema.

Wapo watakaojaribu kuzulumu jasho lako ili lisiwafikie uliowachumia.

Wapo ambao hawatajali maumivu ya wale uliokuwa unawajali nakuwapigania furaha zao.

Amini nakwambia siku ukifa ndio mwisho wa kuthaminika kwa ndoto zako.

Ipo siku utakufa!

Ipo hivyo!

Sijui Kati ya mimi au wewe nani atatangulia lakini naomba nikukumbushe kuwaandaa uwapendao kisaikolojia

Waambie kuwa ni muhimu kujitambua, wajue namna gani wanaweza kusimama hata wewe ukiwa haupo.

Waambie siku ukifa wasitegemee tena kupata mazuri uliyoahidi utawapa katika maisha yako.

Waambie wajiandae kupata changamoto mpya Na wakuenzi kwa mapenzi yao nasio kuongozwa Na wengine.

Waoneshe vitu vyakuvishika siku ukifa, kama ni Mali hakikisha wanaijua Na hatatokea mtu akawanyang'anya.

Kama ni tabia waelekeze utu Na uchamungu, waambie wasimlaumu mtu yakishindikana uliyopanga kuyafanya wewe.

Waambie duniani kila mtu ana Mipango yake ni jukumu Lao kuendeleza Mipango yako nasio kwakutegemea mtu awaongoze.

Waambie washukuru nakumuomba MUNGU kila wanapoguswa Na kutokuwepo kwako.

Waambie wasimdai mtu fadhila ulizowafanyia Na kama ikitokea mtu akaamua kuwalipa basi wapokee kwa kumshukuru.

Wape wosia kabla hujafa!

Waambie bamkubwa yupo lakini huenda akawa Na mzigo mkubwa hivyo akashindwa kuwajali nakuwahudumia mahitaji yao.

Kama ikitokea hivyo wasisitize wasimchukie, wampende nakumuombea huku wakipigania kujikomboa wenyewe kwani ipo siku nawao watakuwa mabamkubwa.

Mwambie mke wako, zilipo hazina zako! Muoneshe viwanja vyako mwambie ni Mali zako, umetafuta kwa jasho lako kwa ajili ya watoto wako.

Msisitize aache uhuni, asije akazihonga! Mtafute mwanasheria kuziwekea hati miliki.

La kama huachi kitu, fukara mwenzangu na mimi! Waambie wanaokuhusu mapambano yaendelee.

Tena uwape Ari watafute kwa juhudi, wasitegemee cha mtu watakumbushwa msiba.

Upendo wasipopewa wasilazimishe kwa kuuomba, cha msingi wajitambue upendo wajipe wenyewe.

Tena washirikiane, kamwe wasiachane, kama wapo wawili faraja wagaiane.

Kama yupo mdogo useme Na mama ake, mwambie awe imara apigane peke yake.

Mueleze ukitakacho, ampe mtoto wako! Mpatie baraka zako uende kwa tabasamu.

Mwambie asilaumu ndugu zako wakimuacha, alee watoto wake kwa shida Na raha zote.

Mkiondoka pamoja mkamuacha mtoto, wala hiki si kioja MUNGU atamkuza.

Atayapata mateso au raha kama ipo, ila mwisho atakuwa maisha ndivyo yalivyo.

Siku ukifa shukuru kama umeacha wosia, waambie wasiutupe radhi itawazuru.

KILA HATUA UNAYOIPIGA WAZA UTAKAOWAACHA BAADA YA KIFO CHAKO.

MUDA NI HUU WAAMULIE WAISHI VIPI BAADA YA KIFO CHAKO.

SOTE TUTAKUFA ILA MKUBWA ANATAZAMIWA ZAIDI....

IPO HIVYO..



Share this

Related Posts

Previous
Next Post »