BLOGU YAKASIRIKA

mwisho wa mwezi wa saba 2016 harakati na shamra shamra zakuandaa uzinduzi wa blogu ya SIMULIZI ZINAISHI (ommyzongo.blogspot.com) zikiwa zimefana kweli kweli, watu wenye kuitakia heri blogu hiyo wakishiriki vema kuitangaza siku ya uzinduzi kila mmoja kwa nafasi yake, ajabu blogu yenyewe yanuna! yakasirika nakuhoji kwanini imetelekezwa! hakuna simulizi mpya inayoandikwa yapaza sauti yake ikifoka eti kwanini juhudi zimeongezwa katika kutangazwa kwake nakufanya watu wengi waitembelee nakuifunua kwa kuigeuza geuza, wakiishangaa kwanini izunduliwe! inahoji kwanini nguvu isingeenda sambamba na kupostiwa SIMULIZI MPYA, yasema imechoka kutazamwa ikiwa haina jipya, yaona hauna haja uzinduzi kama yenyewe haipatilizwi. naishangaa hii blogu nakosa kitu sahihi chakuiambia nataka niishutumu haina shukurani lakini nasita sababu upande mwengine naiona inaongea maneno ya kweli. ni kweli juhudi ziliegemea sana kwenye kuutangaza uzinduzi wa blogu badala kupost simulizi mpya. blogu yase...