Posts

Showing posts from October, 2017

MUHIMU KUJUA @ukweli unaumbua

Image
Ukweli unapotaka kudhihirika kamwe hauwezi kuzuiliwa na nguvu ama utashi wowote alionao mwanadamu. amini nakwambia ukweli una nguvu adimu ambayo haizuiliwi kamwe na vitu kama Pesa, maneno mengi, cheo, huruma wala kujuana. Ukweli ni jambo la kuajabia maana lina 40 zake kama ilivyo kwa siku za mwizi. Ukweli unapotaka kudhihirika haupokei rushwa wala hongo tena humchagua yoyote hata awe ndio bingwa wa uongo siku hiyo hujikuta akianika sura ya ukweli mbele za watu. Ni ukweli pekee ndio ambao huruhusu wenyewe kufichwa lakini unapotaka kujidhihiri hujidhiri wenyewe kwa njia zake. ukweli jambo balaa ambalo nalistaajabia lilivyokaa! maana lenyewe ndio linaruhusu kukumbatiwa na waongo tena wakiruhusu vitu kama Chuki, Uadui, Mauaji, Ubinafsi, Rohombaya na choyo vivae vazi la Upendo, Urafiki, Wema na Kusaidiana na siku ukweli ukijiachia hubaki aibu kwa watu hao waongo. Mra nyingi sifa za ukweli huumiza na ndio maana wengi wetu hatupendi kusadiki mambo ya kweli mbaya zaidi tu...

Dear Septemba....

Image
 "Mwezi ambao nimezaliwa mimi, Mwezi ambao nauthamini, sijui kwanini hua unakuja nakuondoka mwezi huu, September"   Na. Omar Zongo   Unaelekea wapi mpendwa!? iweje unishushe hapa duniani kisha uniache kama hunijui! ninani mwenyeji wangu!? inamaana lengo lako nikunileta kisha unitelekeze!! Jibu lako la jana usiku wakati ukifungusha nguo zako bado nalifikiria eti "nitakomazwa na octoba, novemba na december" hivi mie nawajulia wapi watu hao! niwewe ndio umenileta hapa duniani niwewe ndio nimekuandika kwenye historia! niwewe ndio nakufahamu bosi wangu kwanini lakini unanifanyia hivi!! basi ungeniambia mapema kuwa lengo lako nikunishusha tu duniani halafu utaniacha! ndio ungeniambia namimi nikajiandaa kisaikolojia! nani atanidekeza kama wewe! nani atajua kuwa nimezaliwa katika moja ya siku zako! ninani atajua kuwa nina vinasaba vya baraka zako! hujisikii vibaya labda siku ile unanishusha duniani watu walishangilia kila mmoja akisema "Wak...

chuki shairi

Image
chuki imekuwa vazi,  limewakaa mwilini. kulivua kwao kazi, haling'oki mauongoni kama dunia twapita chuki ya kazi gani. imewakaa mwilini imetuwama nyoyoni. yajionyesha machoni, imegeuka miwani. kama dunia twapita chuki ya kazi gani. chuki pini nyembamba yapenya kotekote si baba wala mjomba atakuchuki yoyote kama dunia twapita chuki ya kazi gani chuki ikikuhadaa pigana kuiambaa ni jumba la karaha sio kiti chakukaa kama dunia twapita chuki ya kazi gani. chuki ina hila zote haingojei sababu ikukuzidia kete itakuvaa taabu hii dunia twapita chuki ya kazi gani dunia hii twapita hatutaishi dawamu litakufika gharika chuki haina nidhamu swali nakuswalika chuki ya kazi gani ulimwengu una adha njiaze kadha wakadha itakupata bughudha fakiri wakujifunza kama dunia twapita chuki ya kazi gani.

SHAIRI: JAWA

Image
"Ni baada tu ya rafiki yangu fulani wakati nipo chuo kuniomba nimuandikie utenzi kumuhusu, kila siku nilikuwa namuahidi nitamuandikia ila siku moja abra ikanishukia na tenzi nikamtungia...." Na. BIN ZONGO Jawa Malkia Zawadiwa Jaaliwa Jawa Tunukiwa pendelewa Zidishiwa Jawa kwani nani mtu gani, ana nini? jawa mwenye hadhi sio mpuzi ni azizi roho yake nyeupe theluji mithili yake sema nini akupe kilicho uwezo kwake haiba ni vazi lake stara jaala yake ucheshi sifa yake maringo hayapo kwake

Wa UBAVU WAKO

Image
Wazungu wanamuita  soulmate je unamjua mtu huyu? umeshakutana nae? unadhani yuko wapi?? anza sasa kumfikiria wa ubavu wako maana ni muhimu sana mtu huyu! kama umempata hewallah laa kama bado fanya hima umtafute mashariki na magharibi usiache akaendelee kuteseka nawe kuteseka kwa nyinyi watu kuishi mbalimbali. huyo ndiyo sahihi kwako, katika mahusiano yako ya urafiki, mapenzi mpaka ndoa. yeye ni muendelezo wa akili zako zinapogota kufikiri! yeye ni msaada wa dhati unapokwama katika hali yoyote! yeye nifaraja unapotokwa na machozi! amini nakwambia ni mtu aaziz sana huyu. hatoruhusu ulie! udhoofishwe na mawazo mabaya na ujihisi mpweke. atakufanya useme "kwanini sikumpata tangu mwanzo mtu huyu!" hata ujinga wake utakuwa ni burudani kwako! yote sababu ni ubavu wako umetokana na yeye wanaoamini uumbaji wa Adam na hawa watasadiki hili kwanini uendelee kuteseka na mtu ambaye hamuendani? kwako wewe moja jumlisha moja ni mbili kwake yeye ni kumi...