AHSANTE MWANA KUJA


Nakushukuru Karima, umpendevu ajabu
Unanifanya nahema, kunipa nyingi thawabu
Ninaipata salama, sia yakutu bawabu
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Ikarima ya Imamu, shauku  tunu amini
Ulinipatia salamu, kwa mikonoko kichwani
Ukaniita binamu, na majina ya utani
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Umenialika kwako, nakuja nafamilia
Nabeba yangu  mifuko, na vibwende navalia
Usije pata shituko, mi sina cha kulalia
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Una nyumba kubwa sana, tarifa nimepata
Yenye viwanja vipana, na kwa kufugia bata
Nina kuweka bayana, usipike vya mafuta
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

situmii vya dukani vinanitoa malenge
Sijapona na  madonda, nilopata mwaka jana
Hapa nipo nimekonda, mzee kama kijana
Pika ninavyo vipenda, vya enzi zetu za jana
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Situmii vya dukani, vinanitoa malenge
Andaa na vya zamani, kama vya kwa mama bonge
Ule mkeka wa utani, ulosukwa kwa mkonge
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Unitandikie chini, nikila na kulalia
Na kiti cha makondeni, sebuleni ntakalia
Zile nyimbo za zamani, nitafurahi kusikia
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Nimesikia tetesi, kwa chombo ki onaona
Wabomoa mkakasi, alojengea Sabuna
Yeye ni fundi wa nyasi, aliyejifunza kushona
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata


Hakika juhudi nzuri, wembamba wakupongeza
Nina yaona dhahiri, na wala sitakubeza
Nakutambua Amiri, usiyejua teleza
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata

Mimi sipendi kasuku, nasikia unafuga
Uwafukuze na huku, wanaiba zetu soga
Uzifute na shabuku, usije nipe mizoga
 Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata



Na, Fulgence Makayula

Comments

  1. nimependa mirindimo,utashi na vibweka
    imenifika muguno,kiswahili kukiteka
    shairi la mikuno,na ujumbe ukaweka
    yakale ndio puno,sasa ni hekaheka
    ahsanteni mwanakuja,salamu nimezipata

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

SEHEMU YA 1&2

UTENZI WA MAHABA

CHIZI MAFANIKIO ; SEHEMU YA 1