Posts

Showing posts from 2022

WARAKA WA JPM

Image
 Huu ni waraka wa kufikirika wa Hayati John Pombe Magufuli, Rais awamu ya tano wa Tanzania ambaye alifariki dunia usiku wa tarehe 17 march mwaka 2021... Muandishi wa waraka huu ni Omar Zongo Kutokea Eneo ambalo wanaenda waliokufa tumepokea waraka huu. Waraka wa JPM. Anasema.... Ndugu zangu watanzania,    ile siku ambayo roho yangu iliusaliti mwili wangu, ilikuwa ndio siku ya kwanza ya mimi na ninyi kutenganishwa katika ulimwengu huu wa Roho na Mwili. Sikuwa na namna yoyote ya kupinga rungu la malaika mtoa roho, ninachoshukuru ni kwamba udongo umeudhibiti mwili wangu lakini Roho yangu ingali hai hata kupata uwezo wa kuyaona yanayoendelea Duniani, lakini zaidi kuwaandikia waraka huu. Nimelazimika kuuandika waraka huu kwa sababu nyingi lakini kubwa ni hili tendo linalotarajiwa kujiri hivi karibuni  Tendo la kuuaga mwaka uliogharimu maisha yangu. Najua nimesaliti kiapo cha Uongozi, kwa kuwaacha kabla ya muda, lakini ningewezaje kupinga mapenzi yake Mungu. Katika waraka w...

Kwaheri 2021

 Wakati unakuja tulikupokea kwa Matumaini makubwa na imani yetu ni kwamba nuru ya mafanikio itatuangazia kwa wingi ndani ya siku zako. Matokeo ya tulichoamini na tulichokitumaini ni siri yetu maana ndani yako tumejifunza kuwa kinywa kinachonyamaza kinaiacha na uzima shingo. Walioshindwa kuficha hasadi zao na kutuonyesha wazi chuki walizo nazo juu yetu ni wengi. Kinachoshangaza majina yao ni ya watu ambao mwanzo tuliamini ni majirani wema. Walioacha kutuamini kwa kuhisi ni wazembe na hatujielewi ni wengi pia. Waliongoja tuanguke ili watucheke hawakukosekana na waliotabasamu kinafki kila tuliponana nao tuliwabaini tukakosa cha kuwafanya. Walioacha kupokea simu zetu kwa kuhisi tutawapiga vizinga ni wengi kama idadi ya waliokataa kujibu meseji zetu kwa kujua kuwa tuna shida. Matendo yetu ya wema yaliyopokelewa kama ni shobo na kujionesha ni mengi kama yalivyo malipo ya dhuluma na chuki tulizoambulia. Mifuko yetu iliposhindwa kununua upendo tukaambulia dharau na kupuuzwa. Juhudi zetu za...