Posts

Showing posts from July, 2018

'Watu'

Image
Kwa tabu sana Mzee alijisogeza juu ya kitanda nakulaza shingo yake kwenye mto. Uchovu wa maradhi ulimdhoofisha vyakutosha, macho yake yaliashiria kukata tamaa, lakini alijikaza kiume. Alinitazama Na kisha akasema. "Ilikuwa ni siku ambayo kila mtu alinisema vibaya nakunizungumzia vibaya, lawama za kila rangi nilipakwa, Hakuna aliyejuwa niwapi nimeelekea nawewe, ulikuwa bado mchanga kabisa. Nimimi pekee ndio nilijua dhamira yakutoroka nawewe siku ile, Kwakweli Siku ile nilikuwa naingojea kwa hamu sana ifike sababu nilidhamiria kuzungumza nawewe. Nilitoroka nawewe nikaenda mbali kidogo Na nyumba yetu, Ulikuwa una siku 40 tu tangu uzaliwe, nafikiri ndio maana watu walinishangaa sana kuondoka nawewe, tena bila kuwaaga. Nilienda nawewe mahala nilipopajua mwenyewe, Ninachoshukuru nikwamba nilichodhamiria kilifanikiwa. Nilizungumza yote na naamini uliyasikia maana hata kawaida yako yakulia siku ile sikuiona kabisa. Ulinyamaza tuli kana kwamba ulikuwa mkubwa kumbe n...

Tafakari Wengine

Image
Muda mwingi hua unautumia kutafakari mazuri yako huku ukihitaji kusifiwa, hua unatamani kuongelewa wewe tu, unatamani kuonekana  Na wote wanaokuzunguka wasifu nakukuheshimu.  Ni nadra sana mtu kutoa nafasi yakutafakari wengine, hivi ndivyo tulivyoumbwa, tumeumbwa na umimi. Unajiona Bora kuliko wengine, wewe ndio unajiona mwenye akili, busara Na ushauri mzuri unaweza kutokea kwako. Ni ajabu sana tabia hii Na kwa vile ni asili ya kuumbwa kwako sina lawama katika hilo Ila leo nataka utenge muda kutafakari wengine, kuona vipawa vyao, nafasi yao, akili zao Na tamaa zao. Ndio, Anza sasa kumfikiria mtu wako wakaribu, ana umuhimu gani kwako. Acha kuwaza wewe tu ndio mwenye umuhimu kwake. Jiulize maswali ya Je ni vipi ingekuwa kama yeye asingekuwepo. Tuanze Na msaidizi wako wa kazi za ndani. Yeye anafua nguo zako, anakupikia, anakufanyia usafi wa nyumba n.k. Acha kiburi chakusema hata kama asingekuwepo ungetafuta mwengine fikiria kuna watu duniani wanatafuta msa...

Mpumbavu 'Shida'

Image
Huna stara, vazi lako ni fedheha, aibu hata huna waadhirisha wazee. Mpumbavu shida. Wafanya mtu awe lofa penye sio aseme ndio, mjinga baradhuli huna utu ata chembe. Ujio wako ni waghafla, hodi kwenu hujafunzwa, harufu yako inatesa pua zote ni madonda. Mpumbavu shida. Kwani kwenu wapi!?? Bosi wako wewe nani, ujio wako washetani ama una baraka za Mungu!? Eti!!, wapendelea nini kwenye maisha ya watu, mbona king'ang'anizi kwenye majumba ya watu!!. Ujira wako upi, kumdhalilisha baba, umefaidika nini kumuandama mama!?? Eti mpumbavu shida!! Nani kakuagiza kwangu, ina maana umeshamalizana na mke wa jirani yangu?? Nani kakupa kiburi,  Shida kuandama watu, hata laana za wahenga shida hazijakupata!! Acha ya mbaraka mwishehe kuna laana ya babu yangu, ulimuandama mpaka kifo shida kweli baradhuli. Okey shida! Keti chini puuza maneno yangu. Zungumza nami Leo nani kakuagiza!?? Kama rushwa nikupe uwaache watu huru! Waache watoto wetu, waache wazazi wetu, waache viong...

Nachora Picha

Image
Hata kama sio mzuri kwenye kuchora lakini Leo naanza rasmi kuchora picha. Picha ya kusisimua, Picha yenye kupendeza, Picha niipendayo, Leo rasmi naichora. Kwanza ile nyumba yangu nnayoiota kila siku. Naanza kuchora kiwanja eneo flani tulivu, upepo flani mwanana, uwanja wake mkubwa. Nachora eneo la kuogelea, eneo lakupumzikia, eneo lakuchezea Na eneo la hifadhi ya ndege Na wanyama Nawachora wanyama, ndege na miti mingi nawaweka humu ndani katika eneo Lao maalum. Nauchora uzio mrefu wa nyumba yangu, nauwekea umeme kuilinda nyumba yangu. Nachora mageti mengi nawaweka Na walinzi nayachora Na magari mazuri ya kila aina nayaweka kwenye 'parking' ya kwenye hii nyumba yangu. Nachora picha ya ndani ya vyumba vya nyumba yangu, kila chumba choo ndani ni nzuri picha yangu.. Rangi flani za amani zinapamba nyumba yangu, ukumbi mkubwa ndani yapendeza nyumba yangu. Nachora samani zote zifaazo ndani, tena zile zakisasa zenye mvuto wa juu. Naichora bahari eneo la mbele...

USIJIELEZEE SAAANA!

Image
We jamaa!! Umerudi home mapema kabla ya mpenzi wako, umekuta nguo zako Na za mkeo zimeanikwa nje!! Umeamua kuanua ili uziingize ndani!! Bila kujua unaanua nguo ya ndani ya jirani yako(wakike), unaingiza ndani. Dakika chache tu jirani yako anagonga mlango, unamkaribisha anaingia, Anaulizia nguo yake kama umeondoa kwenye kamba bahati mbaya, Unamwambia asubiri umuangalize, Ametoka kuoga yuko Na khanga moja tu. Unamlaani shetani, unaingia chumbani nakuanza kuchangua manguo uliyoanua! Unaiona nguo ya ndani ya rangi ya pinki. Unatoka nayo fasta, ili isiwe msala, unamkabidhi. Anatoka nje mara paaap, uso kwa uso na mwanamke wako anatoka kazini. Wivu wa mapenzi unamvaa mkeo, anatazama jirani alivyonona Na khanga moja, anajiaminisha kabisa kuwa ametoka kutenda dhambi Na wewe!! Khanga moja, imeloa!! Mbaya zaidi mkononi kashika nguo ya ndani!! Hata ni mimi nisingeelewa!! Mkeo analianzisha pale nje, anamshukia Na mineno mikali jirani yenu. Jirani mpole,  hajibu...

This Iz My Sister

Image
Na. OMAr ZONGo Hey niaje, naitwa Jayvny, kwetu tumezaliwa wawili tu, mimi na dada 'angu, yeye anaitwa Jackline. Tumepishana miaka sita mimi nayeye!!, tunapendana sana mimi na dada angu licha ya yakwamba tumetofautiana baba. Nataka kukupa kitu chakujifunza Leo kutoka kwa dada 'angu. Sitakwambia amepitia mangapi mpaka kumuita shujaa kwenye Andiko hili ila nitakwambia kuhusu Moyo wake wa chuma. 2014 terehe 01, mwezi wa 11, ndio siku tulimpoteza mama etu, nikiwa Na umri wa miaka 16. Mama aliondoka ghafla duniani, hakupata hata nafasi yakusema 'kwaherini wanangu'. Alituacha mimi Na dada 'angu tukiwa wakiwa, tena wapweke wenye donda kubwa la maumivu ya kifo cha mama etu mpendwa. Nakumbuka kifo cha bimkubwa kilinifanya nilie sana, nilipoteza fahamu. Nakumbuka nilipozinduka nikajikuta nimelala chumbani, kichwa changu kikiwa juu ya mapaja ya dada. Nilifumbua macho kuangaza humu ndani, vilio vya chini chini vilisikika kutoka kwa watu wengi waliomo humu...

Dunia ni jinsia Gani??

Image
Nawaza natafakari, kichwani hoja lukuki!!! Naugua na maswali dunia jinsia gani?? Yakike au kiume, dunia ni dini gani?? Kabila lake mchaga, mnyamwezi au mhehe?? Dunia asili Ipi Iraq ama brazil?? Mwenyeji wa bara lipi afrika ama ulaya?? Dunia yajua nini swahili ama Arab?? Chakula chake ni kipi ni wanga au mafuta?? Yote Mie nayawaza ila kubwa ni hili. DUNIA JINSIA GANI??? Jinsia yake ni KE au ni ME semeni!! Ina hila za kike wakati mwengine huringa! Lakini msimamo wake ni dume, umeikuta na utaiacha. Dunia ina magumu, harakati za kibabe! Tabia hii ni dume, ila utamu wakike. Imehifadhi mengi viumbe aina zote, sifa hii yakike twaitambua wote lakini mbona ni kali yatesa viumbe wake, mwanaume baradhuli hii ni sifa yake.. Dunia kama ni kike kwanini yapendelea, upendo wa mwanamke kotekote waenea. Au tuseme kidume ndio yake jinsia ila mbona pakashume yalea mpaka wambea. Dunia kama ni mama mbona huruma haina, haya tuseme ni baba matunzo yake yawapi?? Kama ni mke iseme ...

Dear tomorrow

Image
Mambo vipi?? Nataka kusema nawewe, imenilazimu kufanya ivo sababu ya hofu uliyoijenga kwa mdogo wangu Sam! Maneno yake mengi kukuhusu ameyaelezea acha nimnukuu "bro, natamani kujua vipi itakuwa kesho yangu, natamani kuona mahali nitakapoanguka, Na jee nitasimama kuendelea Na safari au ndio basi tena, kipi kitajiri kesho nijiandae nacho...nawaza sana!!" Mwisho wakunukuu!! Dear tomorrow!!  Kipi nikupe ili unimegee siri, Je ukifika yatanitokea yaliyonitokea Jana au wewe utakuja namengine mapya!? Je utakuja Na vazi liitwalo huzuni au utaniletea zawadi ya furaha? utasimamia ndoto yangu vema au utaiacha iende Na maji. Nataka dawa ya wanafiki, wazandiki, wachawi waliojificha kwenye mwamvuli wa wema, sasa niambie utakuja Na ufumbuzi wa kuwajua au ndio bado nitaendelea kuishi nao nikidhani ni watu kumbe majitu. Dear tomorrow, nakuwaza mpaka nakonda! Je utakuja Na maradhi yakunilaza au uzima wakuniimarisha?? Utasema namimi kwa upole au utanikemea kwa jazba! Ukija ...

MASWALI Unayojiuliza

Image
 NA Majibu niliyokuandalia!! No1. Nimesoma, nimemaliza nina vyeti smart sana!! Sasa kwanini sina kazi!?? Jibu lake: Kwasababu ulibweteka ukategemea elimu ikufanyie makubwa, ukasahau ulichosomea wenzako mamia wapo mtaani wamesomea!!! Hutaki kujiajiri wala kujitolea kufanya kazi bure, unaamini katika muujiza wakuitwa Na bosi uliyemtumia barua ya kazi!! Unahisi siku moja utakua meneja, kiongozi katika kampuni hiyo, unamuamini mganga aliyekutuma kuku, akakupa hirizi nakukuaminisha utapata kazi hivi karibuni. Shtuka, tafuta njia ya kujiajiri hiyo nafasi unayoitaka kuna mwenzako kaikalia Na amejizatiti kwelikweli mpaka umng'oe basi lazima uwe mzoefu zaidi yake, uwe Na ushawishi zaidi yake lakini zaidi uwe mchawi zaidi yake. Usiendelee kujiuliza swali hili acha sasa Na ubadili mtazamo. No2. Kwanini msichana akiwa Na mvuto sana nakosa ujasiri wakumtongoza!?? Jibu lake!! Kwasababu haujiamini, uzuri wake umefanikiwa kudhoofisha akili yako Na mara zote unajiambia "...

Mchamungu Maskani

Image
leo mcha Mungu nimekuja maskani umenizidi uchungu namkemea shetani enyi vijana wenzangu twendeni ibadani kwani wewe ninani mbona anaturushia stimu zipo kichwani wewe unatuzingua Ibada ndio kitu gani mbona sijakuelewa  Hili kweli nijanga vijana mwateketea Mungu anamipenda ndio mana mewajia punguzeni Maujinga shetani anawaponzea masela hili balaa maskani limeingia jamaa sijui ni njaa msikie anachoongea oyah hebu ambaa tusije kukuchengua huruma nawaonea enyi vijana wenzangu nawaomba zingatia nasaa hizi zakwangu nyakati zimewadia anawahitaji Mungu Mungu ndio kitu gani lini ulimuona akija mambo ya kizamani maskani toa kioja Mungu wetu mjani kamatia pafu piga Mungu awasamehe hamjui mlisemalo shetani tumkemee hatapata atakalo acheni niwaombe enyi mabarobaro shika adabu yako muombee mama ako hatutaki sera zako ni hora uende zako sura ka mbwa koko fanya usepe zako. maarifa ndio hamna basi pokeeni yangu nafanya kila namna kuwaokoa w...