Posts

Showing posts from April, 2018

UONGO WA MAMA 'ANGU

Image
Ni Simulizi niliyoitohoa kutoka kwenye clip flani iv yakizungu. Nimeweka Utashi wangu ili kufikisha ujumbe kama uliokuwepo kwenye clip ile, sijacopy nikapaste, kuna vingi nimebadili kuleta uhalisia... Na. Omar Zongo "Usihuzunike, sihisi maumivu, najiona nina afadhali!" Huu ndio ulikuwa uongo wake wa mwisho kuniambia!! Baada ya hapo alifumba macho na hakuweza kufumbua tena. Roho yake ikaacha mwili! Leo ndio nakumbuka, mama yangu alikuwa Muongo, hata kabla ya siku hii ya mwisho. Nakumbuka, wakati mdogo, mara nyingi chakula chetu kidogo kinachopatikana, yeye alikuwa hali na alikuwa akisema  "nimeshiba kijana wangu, kula wewe ushibe!" Nilikuwa namshuhudia akiokoteza mifupa ya samaki niliyobakisha mimi. Hata nilipokuwa nikimbakishia minofu ya samaki alikataa kabisa akisema hapendi samaki!! Nilipoanza shule ya awali, ilimbidi afanye kazi mbilimbili ili aweze kumudu ada za shule. Hakupata muda wakupumzika! Mara zote nilipokuwa nikishtuka us...

ANDIKO TATA

Image
Na. Omar Zongo Hili ni andiko Tata tena tupu, linalosindikizwa na ala ya simanzi! Linajichora kwa kalamu ya ukiwa kwenye karatasi ya upweke. Andiko lenye nukta ya kilio na koma ya kukata tamaa!! Andiko lenye madoa ya machozi na uchakavu wa kilio. Mwandishi nimie mkiwa mwenye tamaa ya nuru, niliyesimama njia panda mbele kiza, nyuma miba, kulia moto, kushoto mamba mwenye njaa! Mwandishi mchovu mwenye akili ya majuto! Kosa langu silijui lakini najihisi nina hatia. Duniani wakumlaumu nadhani nimimi mwenyewe!!. Naandika ilhali nina uchovu ila kwa vile ukamilifu wa Andiko nautaka siachi kujihimu niendelee ingawa kwi kwi za kilio zanikosesha umakini. Ni ipi tamati ya Andiko!! Je ni kusagwa na meno ya mamba au kushambuliwa na ncha za miba??? Je, nikupata joto Kali la moto au kupotelea kizani!?? Ninani msaidizi katika hatua yangu ijayo??? Ninani mpatanishi wa mgogoro wa nafsi yangu!?? Je nimimi mwenyewe au kudra za Mungu!?? Je ni rafiki ambaye simuoni au ndugu aki...