NIMEZAMA TOPENI

uvundo nausikia, karaha tupu puani. tope hili madhara, afya yangu hatiani. sinayo hamu yakula njaa ingali tumboni. ninani wakunitoa nimezama topeni! siwezi kujinasua tope limeniganda nashindwa kujiondoa,kihoro kimenipanda. masaa yanasogea joto lazidi kupanda tope lanizidia mwili wote waganda tope hili maajabu launguza mwili wangu nimepuuza ya babu na sasa majuto yangu ubishi ndio sababu wahaya mateso yangu, nani sasa wakutibu matope mwilini mwangu. sina wakumlaumu kadhia mejitakia tope hili lasumu nimezama kwa umbea! sinayo tena hamu, mecheza pata potea meupata ugumu kwa nnayojionea ombea yasikupate,utageuka msongo. niliambiwa ningoje nikaona ni porojo, nikauvaa mtope sasa wanipa kipigo zamishwa mwili wote iliyobaki ni shingo tope flani karaha, kulijua ni vibaya limejua kunihadaa bila soni wala haya chini yake nimekaa, siwezi tena kimbia maumivu majeraha nafsi yangu yajutia mwanzo niliona tamu kuchezea tope hili, lilinikidhi na hamu, sikuiona shubir...