Posts

Showing posts from July, 2017

USISAHAU CHANGAMOTO @UjanaMajiYamoto

Image
Na.  Omar Zongo Ishi nami kwa furaha ila tambua siku moja kuna karaha hivyo usisahau kujiandaa! Usisahau changamoto ambazo kwa jicho langu naziona zimejaa pomoni! kupendana angali vijana ni suala lamaana lina taadhima na kubwa heshima! lakini usisahau kuwa ujana ni laana, jumba la usahaulifu na upotofu na kwa taarifa yako wengi waliouvamia sasa hivi ni wafu! walio hai wanasubiri andiko litimie!, afya zao dhalili, wakenda kama walevi, wamedhoofu mwili, nguvu zao kumbukizi, kwao naona dalili ya kupoteza nguvu kazi, ni baya suala hii UJANA kweli maradhi. Usisahau changamoto ya kwanza kwetu Ni Ujana! tena hii ni ya Moto yapasa kuomba sana. tuvuke mito, vijito tukeshe kuombeana! kwenye baridi na joto tubaki tumeshikana. Tena tuache utoto laa sivyo tutaachana. Ujana ni changamoto naomba kumbuka sana! wengi eti tulizo wanasema lipo kwa wazee! eti "vijana mzozo bora tuwapotezee" mapenzi sio mchezo yanaumiza aisee! singeni khabari hizo mchumba uzireje...

USINIACHE MUNGU WANGU!

Image
Naandika kwa mtindo wa kuomba, maombi ambayo yametawaliwa na unyenyekevu na sura yangu ina dalili zote za kuonesha kuwa nina uhitaji wa ninachikiomba! tena sio uhitaji mdogo nina uhitaji mkubwa wa nikiombacho leo. Yupo mpumbavu mmoja, ambaye daima sura lake analikunja kwa jazba kila anaposikia nataja jina lako kwa unyenyekevu nakumuita yeye kwa kiburi tena nikimtukana kumuita Mwanakharamu. ni yeye ndiye ambaye ananitamani kuninyakua nakuniadhibu vikali, anatamani niwe mtumwa wake, ananiwinda kwa juhudi zake zote na hata siku moja hajachoka kunifatilia. ni huyu maaluni ndio leo amenifanya ninyooshe mikono yangu kwako nikiomba kwa unyenyekevu nikikusihi kamwe usiniache maana dude hili linanitamani leo kesho niwe rafiki ake. lengo lake nikuasi Mungu wangu na nifanye yale uloyakataza hakika nakuambia sijawahi kumpenda kiumbe huyu tangu nilipoijua dhamira yake kwangu. leo nina machache nataka kukwambia MUNGU wangu na nakuomba sana unipe msaada wako kwa kuniitiki...

MASIKINI "MSAMAHA" @thamani yako haipo!!

Image
uko wapi rafiki yangu msamaha, kusema kweli nimegundua leo kuwa haupo katika dunia hii maana mimi mwenyewe nimeshindwa kujisamehe mpaka muda huu kwa uzembe wakupoteza andiko langu la mwanzo. Na Omar Zongo Andiko langu lakwanza kukuhusu lilikuwa zuri lapendeza nililipamba kwa vazi la mafumbo juu yake nikalivika joho zuri la tenzi kisha nikalipulizia marashi yenye misamiati ya lugha adhimu ya kiswahili! ndio!! andiko kukuhusu wewe MSAMAHA nililipamba likawa kamili kwa kusomwa lakini sijui ninini masikini ya MUNGU ghafla bin vuu tsunami la teknolojia ya simu inayohitaji chaji kuwa pomoni muda wote likanivaa simu ikazima kabla ya andiko langu kukuhifadhi ukahifadhika. kwa namna ambavyo nilikupangilia ukapangika wallah naapa sikuwahi kupangilia vizuri andiko lolote kabla yako! nafsi ikiwa imejawa lawama yakutokuwa makini na chaji yangu nikakumbuka kujiomba msamaha na nilipofanya hivyo angalau nafsi ikawa huru lakini nikaja gundua kisasi na simu yangu hakikuniisha moyoni nil...

KESHO HAIJULIKANI @Ishi Ki kamilifu

Image
Na Omar Zongo Siku za mwisho kabla ya kifo chako nakiri niliona mabadiliko ya kitabia! ulipenda kukaa mwenyewe! upole ulikuvaa na hata chakula kilikuwa hakipandi jambo ambalo silakawaida kwako, kiukweli upweke niliuona kupitia macho yako na sijui kwanini nilikupuuza. leo natamani kujua nini chanzo cha wewe kuwa hivyo lakini sina namna yakusikia sauti yako ikinieleza. je ni hali ngumu ya maisha ulikosa dira na muongozo??? mimi sijui.. je ni mapenzi yalikuvuruga kiasi kwamba ukakosa ushauri wangu mimi kaka ako hivyo ukaamua kujimaliza??? hili pia mimi sijui wakati mwengine nawaza labda kutokuwa karibu tena nawewe tukibadilishana mawazo, kucheka na kutaniana ndio chanzo maana ni ukweli kuwa ulinizoea sana na ni mimi pekee ndio nilikuwa kaka na rafiki yako pia. bado hili nalo sina uhakika nalo pia. kwa ufupi nateseka kwa kutaka kujua kilichokufanya ukakatisha pumzi yako. sijui kwanini sikutilia maanani nilikupuuza uliponiomba kuzungumza nami hata sauti yako iki...

TWENDAPO WAZEE HAWATAKUWEPO!!!

Image
"Huko twendako, siku baada ya hizi nina uhakika wazee watakuwa viumbe adimu kuonekana katika sura ya dunia hii! sababu ni nyingi lakini chache kati ya hizo ndizo nitakazoziwekea mkazo katika andiko langu la leo!" Na Omar Zongo Baridi kali inayopuliza mwilini inasababisha mwili usisimke kwa woga vinyweleo visimame, hali hii ya hewa ni sababu tosha kwa wavivu kuvuta shuka hasa mishale hii ya asubuhi lakini kwangu ni tofauti, saa kumi kamili za alfajiri niko macho natafakari utashi wa MUNGU. tafakuri yangu hiyo inaenda sambamba na vitendo vyangu takatifu vyakujiandaa kwenda masjid kumsujudia mwenye dunia hii, mwenzenu imani yangu ni muislamu lakini namshukuru MUNGU sijawahi kukashifu imani za wengine. vitendo vyangu vya maandalizi yakujiweka safi kimwili na kiimani vinachukua kama dakika kumi na tano hivi, najipuliza marashi, navaa msuli wangu kwa kuukunja vema mkwiji, shati langu safi nililoliandaa kwa ajili ya swala ile kisha nalisindikizia na koti ku...

SAUTI YA MUNGU

Image
  Anaandika  Omar Zongo wakati mwengine ukiwaza sanaaaa utagundua kuwa hauna faida yoyote kwa mwenzio wala yeye hana faida yoyote kwako! ukiendelea kuwaza sanaa utagundua ni MUNGU pekee ndio mwenye faida kwenu wote, na ukiendelea kuwaza sanaa utagundua mnashobokeana, kufuatiliana kujuliana hali na kujaliana kutokana na Amri ya huyo  MUNGU ambaye ametuamrisha tupendane na ni dhambi kuchukiana. ukiwa unaendelea kuwaza sanaa utazidi kubaini kuwa anaekupuuza kutojali uwepo wako na kukupotezea hauna sababu yoyote yakumshobokea, kumfutalia nakumjali lakini ajabu ukiendelea kuwaza sanaa utagundua kuwa kufanya hivyo nikumuudhi MUNGU wako ambaye anakujali wewe kwa ukarimu mkuu! na niyeye ndiye aliyekuamrisha umpende adui yako! ukiwa hujachoka kuwaza utagundua kuwa kuna kitu kinaitwa uvumilivu kinahitajika sana ili uwende sawa na watu wote maana wameumbwa kwa mitihani usipoangalia unaweza ukaamka asubuhi moja nakuwatukana wote kwa kuwa hawana faida kwako! ukiwa unaendelea k...

NIHESHIMU MKE WANGU

Image
Unakumbuka maisha yako kabla sijakuoa?? ulikuwa hauna tofauti na bidhaa yakukodiwa ambayo ilikuwa ikitumiwa nakurudishwa ili mwengine aje aikodi tena. maisha yako yalikuwa na uhuru wakukudharaulisha. wapo wanaume wengi kama mimi walikufata nakukutumia bila hata kuwaza kuwa unastahili kuolewa. kitendo cha mimi leo kutimiza ahadi yangu nakukuoa kinatosha kabisa kufanya wewe uniheshimu. sio kama sijaona mapungufu yako au wewe ndio mwanamke mkalimilifu kuliko wote laa hasha! nimekuoa kwasababu nimeamua kukupokea kwa jinsi ulivyo so inatosha kabisa wewe kuniheshimu. kwani hujasikia fununu kuwa duniani wanawake mpo wengi kuliko wanaume sasa kwanini usione bahati kubwa kwako kuchaguliwa namimi nakuolewa eti huoni kuwa nastahili kuheshimiwa nawewe?? Niheshimu mke wangu sababu nahisi kuwa nimekuvisha stara nakukutofautisha na wanawake wengine wahuni wanaotumiwa nakuachwa kila siku, naamini kuwa hayo sio maisha mazuri yanayompendeza binti yeyote hivyo niheshimu mume wako ...

MWENYE SIFA HIZI AJE!!!

Image
Awe na kinywa tulivu chenye ulimi asali, neno lake tulizo sauti yake gitaa. umbo lake pambo, mvuto kwa jicho langu, rangi ladha tamu si mweupe si mweusi! lafudhi yake wimbo lahaja iwe ya pwani, sikio lipumbazike aniitapo jina. aniduwaze na mwendo mithili yake hapana kaumbwa kwa mapambo na Mungu wa sifa njema. upole tabia yake si binti wa pekepeke imani vazi lake hofu kwa Mungu wake. kajaaliwa midomo unene wa kitumbua jicho lake legevu MUNGU kalipaka kungu. nijione Adamu naye ndiye Hawa Wangu tena anipe faraja tabasamu lake afya. Ngozi yake mboga wala sio yakughushi mchicha na matembele si maji wala mchina. kauli yake dira, upole ndo vazi lake wala hawezi kuzira subira tabia yake. roho yake imani, uchamungu matendo yake, adui yake shetani tumaini lake MUNGU. mwenye sifa hizi nani namgojea afike simtaki hayawani akija nifilisike. sitaki jibu dhalili eti nimuumbe mwenyewe naahidi kumsubiri hata kama yu tumboni. akijue kiswahili maneno yake matamu, kizungu sist...