Posts

Showing posts from June, 2017

JUNIOR

Image
 "Sikuwahi kusimulia kisa cha kweli nikakiruhusu kusomwa na watu pengine hii inaweza kuwa simulizi yangu ya kwanza yenye ukweli ndani yake, ni zawadi kwa ndugu yangu Ramadhan Madebe ambaye kwa asilimia kubwa amechangia ukamilifu wa simulizi hii....ni sehemu ndogo pekee ndio yakubuni lakini mengi yana ukweli....." JUNIOR SEHEMU YA KWANZA Niliona wivu sana baada ya rafiki yangu kupewa jina na dada yako, yeye aliitwa mwinjuma lakini alimbeza jina lake hilo na akasema kuwa anapendeza zaidi akiitwa Geminus! Leo ndio nagundua kuwa aina ya familia bora kama ilivyo ya kwenu ndiyo huwaaribu watoto nakuwafanya wayachukie majina ya Kiswahili kutokana na wao kukesha wakitazama filamu za kizungu na kihispania. Hata kama muhusika mkuu katika filamu ya kizungu akitokea anaitwa Zongo, mradi ni mzungu na anacheza vizuri kwenye nafasi yake basi jina hilo linaweza kuwa ni jina zuri kuliko yote duniani. Kiukweli licha ya kuwa akili yangu ndogo lakini imebaini kuwa hili ...

UMESAHAULIKA BABA WA KISWAHILI

Image
Imekuwa ni desturi yangu kuenzi harakati zako kila siku hasa kipindi ambacho ni kumbukizi ya kifo chako mithili yakuzima kwa mshumaa uliokuwa ukimulika fasihi andishi yenye tija na akili kubwa kwa miongo kadhaa sasa yaani tangu na baada ya kifo chako. Baba wa kiswahili, Shaaban Robert  (kuzaliwa 1 January 1909 – kufa 20 June 1962) Nionacho leo kuhusu kuenzi mchango wako ni USAHAULIFU MKUU, kiukweli UMESAHAULIKA BABA WA KISWAHILI!  Anasimulia Omar Zongo  Naona aibu kusema kuwa natamani ule utashi wako walau ungeuacha sehemu kisha ukaniagiza hata ndotoni nikauchukue niutumie kuendeleza falsafa zako na utamu wa Kiswahili uliopo ndani yako. Nasikitika ninapogundua kuwa 20 june wakati unafariki ulikusanya kila kilicho chako nakuelekea nacho kaburini, sitaki kusema kuwa hilo limetokea kutokana na uchoyo wako laa hasha ila nakulaumu kwanini hukutaka kumuachia mtu arithi angalau robo ya unguli wako wa kutumia vema hii lugha Kiswahili katika maandishi. Ni...

KIZIMBA Cha IBILISI

Image
Ilipoishia sasa Nikawa namshuhudia Ramadhani akifungua lango lile la Kizimba cha Ibilisi…wasiwasi na kihoro vikanivaa sikuamini kuwa ni mimi ndio naenda kumuona Ibilisi huyo mjaa lana. Sasa endelea Kidokezo SEHEMU YA PILI "Tangu kufika kule juu ambako nilielezwa kuwa ni mbinguni sikio langu lilikuwa linapokea taarifa za ajabu tupu, kama ni somo hakika lile nilibahaika kulisoma pekee yangu duniani, nilizidi kumfurahia Ramadhani, nikajikuta namuuliza “Sasa vipi hapa tulipo hawawezi kutuona?" Na  Omar Zongo Chumba kile kilikuwa kidogo ambacho kilimtosha Ibilisi peke yake, aliviringishiwa minyoror mwili mzima ili kudhibiti vurugu zake zakutaka kutoka kifungoni pale. Kwa harakaharaka niliyachunguza mazingira ya mule ndani nikabaini kuwa kuna joto kali mno, kiasi cha muda ule mchache tu nikawa tayari nimelowa mwili mzima kwa jasho, nilijiuliza Yule ibilisi anawezaje kukaa mule. Kama vile Ramadhani alijua nini nawaza akajikuyta ananipa jibu “mahala ...

KIZIMBA Cha IBILISI

Image
SEHEMU YA 1 "Habari hii nilikuwa naisikia sana kwa watu wa Mungu hasa masheikh duniani wakisema kuwa Shetani hufungwa wakati Ramadhani inafika lakini ilikuwa haijanisisimua kama alivyoniambia Rafiki Yangu Ramadhani, chuki dhidi ya huyo kiumbe aitwae Ibilisi ikanivaa, sasa nikawa natamani kumuona"  KIZIMBA cha IBILISI Na Omar Zongo Anaitwa Ramadhani, rafiki yangu asiye na ubaguzi, mpole mnyenyekevu na mwenye kufundisha mema! Hakika sikuwahi kujuta kufahamiana na Mja huyu mwenye kila dalili za utu wema. Kinachoniuma zaidi ni licha ya kuwa ni mwema na ningependa kuishi nae milele lakini desturi yake ni kunitembelea mara moja tu kwa mwaka na   hakuna namna ambayo naweza fanya kubadili desturi yake hii. Miaka yote anakuja naishi nae akinifundisha namna yakuishi kwa kufanya matendo mema yenye kumpendeza Mungu muumba aliyenifanya mimi nikawa kwa amri ya neno lake moja tu, miaka yote namfurahia Ramadhani lakini mwaka huu nimefurahia zaidi ujio wake maana amewe...

EL PERDEDOR

Image
“Wanaume ni watashi sana katika kutumia nguvu na mabavu yao kuwanyanyasa wanawake, lakini sijui kwanini wanashindwa kutumia utashi wao huo kutambua thamani na upendo wa mwanamke anayempenda kwa dhati.   Kuzidisha drugs watu wanaweza sema ndio chanzo cha kifo chako shoga angu lakini mimi nasema mapenzi ndio chanzo...naamini nafsi yako itawaadhibu wanaume wote wenye moyo kama wa aliyekufanya uwe marehemu leo hii, Rest In Peace shoga angu, nitamiss kukuita hivi madia...”  EL PERDEDOR Na Omar Zongo Uliniumiza kichwa sana nilipoona mchoro wako ulioonesha mwanamke amejiinamia kisha ukiambatanisha na neno hilo El Perdedor. Niliwaza nikawazua nikijiuliza unamaanisha nini, nilijihoji je ni jamaa mwengine umempata ambaye amekalia kiti cha huba kilichopo moyoni mwako ndio anaitwa jina hilo?? Lakini nilijikosoa maana kama ni jamaa mwengine kwanini uliweka picha yako ukiwa umeinama, kulalia magoti. Nikajiuliza tena neon lile linatoka kwenye lugha gani   maan...