Posts

Showing posts from April, 2017

NAKUSHIKA SIKIO

Image
Aliposikia hatua za mtu akaongeza umakini nakusogea karibu, ghafla akashtuka paji la uso wake likitobolewa na vyuma vya moto, alikuja kugundua baadae kuwa ni risasi ndio zilipenya kichwani mwake, mwili wake ulianguka chini mithili ya mzigo... ni hapa ndipo alipongundua SIKIO LAKE LIMEMPONZA kusikiliza hatua za watu hatari na wakatili kiasi kile....alijilaumu kwanini asingepuuza kusikia hatua zile lakini majuto yake hayakuweza kusaidia roho yake isitoke...sasa alikuwa chini akipigania roho yake ambapo dalili zote za kifo tayari aliziona... SIKIO LILIPONZA ROHO YAKE! nina kila sababu ya kuzungumza na SIKIO LANGU!. Nakushika sikio! Na Omar Zongo Sikio langu ni dira nzuri ya kuupima muelekeo wa ngurumo za sauti zitokazo pande zote za dunia hii. leo nasema nawe sikio maana namini wewe ndio kiungo pekee ambacho utanifanya ule umimi niliozaliwa nao, nisiupe nafasi kuwa kero kwa wengine. usikasirishwe na mabezo ya watani wangu wanaodai nina sikio kubwa ka' upawa wa uji,...

RUDI KAMA IKITOKEA, MAMA....!

Image
"ISHI UKITAMBUA KUWA WAJA WALIKUJA WAKAWA NA KISHA WAKATOWEKA! NA HIVYO NDIVYO ITAKAVYOKUWA KWAKO NA KWANGU! TUTAACHA HISTORIA. HAKIKISHA INAKUWA HISTORIA YAKUIGWA"  Na.  Bin Zongo Kama ikitokea nafasi iliyo ngumu kutokea kama yalivyo mapigo ya moyo kwa mfu,itumie! usiikatae hata kidogo, hakikisha nafasi hiyo inakuwa ya kwako, imiliki na urudi tena maana ule upenyo uliouacha mithili ya pengo bado hauna namna yoyote yakuzibika. sijui utofauti uliopo kati ya hapa ulipokuwa na huko ulipo sasa, lakini naamini wewe ni shahidi wa kitu kilichopo hapa kiitwacho 'bahati' kama ikitokea kitu hiki ama kinachofanana na hiki kinakudondokea kamwe usisite kukiokota. naomba sana ukiokote kwa juhudi huku ukitambua kuwa tendo hilo ni msaada mkubwa kwangu yaani mithili ya ngumi nzito itakayomdondosha chini adui huyu aliyenizonga mwenye jina la Upweke. nidhihirishie upendo wako! upendo ule ambao mpaka leo sijapata mfanowe, naomba unidhihirishie kwa kutumia nafasi hiyo itak...

IPO SIKU NITADONDOKA

Image
"Safari ya kifo ni safari inayoumiza sana maana ina nguvu kubwa isiyoweza kupingwa na matakwa yako, ni mithili ya kuisha kwa mshumaa au kuzama kwa jua, ULAZIMA WA SAFARI HII NDIO UNASISIMUA NAKUSIMAMINZISHA MNO...lakini hakuna jinsi naomba niukubali ukweli IPO SIKU NITADONDOKA" Na Omar Zongo Kamwe usije kusema utaniokota sababu safari hii ni ya kificho, hajulikani ni nani wa kuanza na nani wakumaliza. sote tupo matayarishoni na huo ndio upekee wa safari hii, mimi nikidondoka ndio kipindi ambacho simulizi zangu zitasisimua zaidi kuliko hivi sasa na Pengine uthamani wake utaongezeka zaidi. ipo siku ingawa siijui ni lini lakini naamini nitadondoka! Wapo ambao watashtuka sana huku vichwa vyao vikirejea wasifu wangu na namna nilivyokutana nao nakufahamiana nao. Nina uhakika siku hii itakua ni yakutaja mazuri yangu tu na hata walionichukia bila sababu za msingi watabaini kua sikuwahi kuwakosea mpaka wanichukie namna hiyo, hapa ndio watajua sikuwahi kuwa na makosa nao...

MZEE BABA

Image
Mzee baba shikamoo mzee wangu, mzee baba!! naheshimu sana uwepo wako ndani ya kaya hii ambayo ilipoteza kabisa heshima yake tangu kufariki kwa Baba angu mzazi. kwa muda wote tangu pigo la kifo cha baba angu mama amekabiliwa na maadui wengi wakiongozwa na DHARAU, ambaye kila uchwao alikuwa akifanya kaya yetu ipuuzwe sababu ya UJANE wa mama.  eti waliamini mwanamke pekee hana sababu yakuheshimiwa. walikuja mababa wengi kila mmoja na namna yake aliyoitumia kumlaghai bimkubwa, wengi walikuwa hawasimamii uanaume wao ndani ya nyumba. nimegundua mzee baba wewe unafanikiwa sana kwasababu ya ule mtindo wako wakujiuliza kila mara 'JE MIMI NI MWANAUME??' wengi wanakusema vibaya eti mama anapata shida sababu wewe una chembechembe za mfumo dume lakini amini au usiamini mimi mtoto wa pekee wa kaya hii nakupa pongezi na wala sijaona kibaya unachofanya kwa mama angu mzazi ambaye mara zote mwenyewe anaongozwa na ile jaala yake ya upole na bashasha lake la amani usoni, ama...

SEHEMU YA 1&2

Image
SEHEMU YA KWANZA ''Ni kawaida kwa hadithi nyingi pendwa kuwa na sehemu ya kwanza na sehemu ya pili na nyengine nyingi zenye mfululizo wa visa vya kusisimua, lakini ukweli wa mambo ni kuwa hali ni tofauti katika mapenzi, Hadith ya mapenzi inayonoga zaidi ni ile ya sehemu ya kwanza, ukiiharibu kwa kudhani kuwa utapata sehemu ya pili ni kosa kubwa sana ni sawa na ufa usioweza kurekebishika'' HII HADITH HAINA JINA INAITWA SEHEMU YA KWANZA NA SEHEMU YA PILI..... NI KISA CHA MAPENZI ..... Na  Bin Zongo   Mapenzi yamekolea hakuna aliyeona kero kwa mwenzie, kila mmoja anaishi kwa amani na hutabasamu kila wakati akikumbuka uwepo wa mwenzake. marafiki zao walikuwa wanawaona machizi mana walipokuwa mbalimbali kila mmoja alikuwa busy na simu yake akichart na mwenzake nakucheka cheka kila saa kama chizi mpya aliyepelekwa kituoni kwa matibabu. mapenzi yao yalikuwa yanavutia kama mapenzi ya kitabuni, yalifanya kila mmoja kati yao aone thamani yakuzaliwa kwake, nafs...

SHEM UNAMUUMIZA SISTE ANGU AUDIO

Image