UJUMBE KWA WAKWE ZANGU

''Katika dunia yetu ya leo malezi ni suala ambalo halipatilizwi sana, wazazi wamekuwa wapuuzaji hivyo kufanya vijana wa kiume kutotambua maana ya uanaume wao na vijana wa kike kutoiona thamani yao, kama muandishi nimeona haja yakukumbushia suala la malezi kwa mtindo huu...ifuatayo ni barua kwa wakwe zangu'' Na BIN ZONGO Bado sijaoa lakini naamini ipo kaya moja duniani hapa anaishi mwanamke nitakayemuoa na pengine analelewa na wazazi wake Ujumbe huu nataka ufike kwao... Ujumbe huu uwafikie wakwe zangu na najua mtastaajabu sababu bado binti yenu hamjamuozoesha wala pia barua ya posa hamjapokea. me naamini ninyi ni wakwe zangu na sitasita kuwaita hivi sababu wahenga walisema NDOA HUFUNGWA MBINGUNI. mimi na binti yenu tayari tumeshafunga ndoa mbinguni hata kabla nafsi zetu hazijaletwa hapa duniani. nimewahi kuwaletea waraka huu wa barua ili kuwajulisha mengi ninayoyataka muyafanye kabla sijakutana na binti yenu. naandika ujumbe huu nikiwa sina hata...