Posts

Showing posts from February, 2017

JIKANE SASA

Image
''jikane kwa pigania maneno kama vile anaringa, ana roho mbaya maana  maneno hayo tafsiri yake ni nzuri kwa nafsi yako yaani nikwamba unajiamini na njia zako na unapambana kwa mafanikio yako kwa kushirikiana na wachache ambao utaamini wao wanakustahili, unaendana nao na wana msaada mkubwa wakukufikisha unapoota kufika''   Na. Omar A. Zongo Waheshimiwa wahenga walisema kuwa utendapo wema, nenda zako kamwe usingoje shukurani. wakaibuka wengine wakatanabaisha ni busara mkono wakulia ukitoa wakushoto usibaini. wakaja wengine wakaunga mkono kwa kusema wema wa aina yoyote hauozi. ahsante waheshimiwa wahenga, nasadiki lakini zaidi naheshimu mawazo yenu yalo busara pomoni. kilembwe wenu leo naibua hoja ikiwa ni namna nzuri yakuheshimu fikra zangu nakuzithamini maana nimejaribu kuangaza dunia yote hii sikuona wakuweza kuthamini mawazo ya wengine maana ni watu wa dunia hii ndio walio jaaliwa dharau nakujiona wao na watu wao wanaowahusu ndio bora kimawazo. sijawah...

MTU NA MTUWE; SEHEMU YA 2

Image
"Zawadi nzuri ambayo nipo nayo na nitakuwa nayo daima ni talanta ya uandishi niliyojaaliwa na Mungu, nalazimika kukuzawadia simulizi hii nzuri ya Mapenzi katika msimu huu wa Mahusiano mema kwa wapendanao, msimu wa valentine day, NI KISA CHAKUBUNI AMBACHO NIMEJITAHIDI KUKIMEGA KATIKA SIMULIZI YANGU NZIMA IITWAYO MTU NA MTUWE, NIMEWEZA KUMEGA BAADHI YA VIPANDE NIKAPATA SEHEMU YA KWANZA NA YAPILI.....SONGA NAYO SEHEMU YA PILI YA MTU NA MTUWE'' Na.  OMAR A. ZONGO Ulikuwa ni usiku wa maajabu kwangu, usiku wa vituko na nyingi tashtiti za mapenzi. usiku wakuamkia SIKU YA WAPENDANAO, nikatika usiku huo ndio ambapo taarifa niliyoisikia kwenye kituo cha luninga cha CNN niliamini kuwa ina ukweli sasa wazi nilijionea hali ya mambo, nikweli siku ya wapendanao ya mwaka huu ilikuwa ya ajabu. KILA MTU ATAMFUATA ANAYEMPENDA KWA DHATI. tayari Victoria alinifata mimi huku mimi nikimsihi Jamila wangu atulie wakati Jamila mwenyewe alishamkumbuka X wake aitwae Edy. tayari saa sita...

MTU NA MTUWE; SEHEMU YA 1

Image
"Zawadi nzuri ambayo nipo nayo na nitakuwa nayo daima ni talanta ya uandishi niliyojaaliwa na Mungu, nalazimika kukuzawadia simulizi hii nzuri ya Mapenzi katika msimu huu wa Mahusiano mema kwa wapendanao, msimu wa valentine day, NI KISA CHAKUBUNI AMBACHO NIMEJITAHIDI KUKIMEGA KATIKA SIMULIZI YANGU NZIMA IITWAYO MTU NA MTUWE, NIMEWEZA KUMEGA BAADHI YA VIPANDE NIKAPATA SEHEMU YA KWANZA NA YAPILI.....SONGA NAYO'' NA. OMAR A. ZONGO Mie na valentine wangu tulikuwa nayo desturi yakutazama habari za ulimwengu kupitia Shirika la utangazaji la CNN. hii ilikuwa ni asubuhi mishale ya saa ni saa kumi na mbili. miongoni mwa habari zilizonishangaza ni ile iliyosema kuwa eti Siku ya wapendanao kwa mwaka huu itaadhimishwa kwa maajabu makuu. Habari hii ilieleza kuwa kutokana na dhulma na kuibiana wapenzi mwaka huu mioyo ya watu imeamua kufunguka na kueleza kwa vitendo ni yupi anapendwa kwa dhati. habari ile ilisema kuwa uongo wote katika mapenzi utakoma siku ya tarehe 14...

USIMUAMINI

Image
Bora tu kuwa muwazi nakupinga uongo wakumpamba kwa maneno mazuri yanayomfanya umuone mwema! fungu utakaloniweka utajua mwenyewe ila mimi nakuambia ukweli USIMUAMINI! ndio, usimuamini kwa lolote asemalo labda akuthibitishie kwa vitendo nawewe ujiridhishe kweli ametenda yeye maana uongo upo hata kwenye utendaji! tangu kuzaliwa kwake jicho hili limeona mengi nakujifunza vingi pia, moja ya fundisho ndilo hilo nakuasa nalo KAMWE USIMUAMINI! nimuongo, mzandiki na mjanja kupindukia ukiyaamini majibu yake hakika utapotea, suala la msingi ni moja tu usimuamini! kama huniamini hebu Tafuta vitabu vyooote vya mapenzi na usome hulka za wapendanao nina uhakika hakuna hata mmoja aliyewahi jibu kuwa sio muaminifu pindi alipoulizwa na mwanza wake kama ni muaminifu! uhakika ninao kila mmoja hujibu kuwa yeye ni muaminifu tena wa kiwango cha juu tena ubaya zaidi huweza hata kupitisha kidole chake shingoni akiapa kwa jina la MUNGU wake kuwa yeye ni muaminifu wakati ukweli sio huo! hata HOFU ya MU...

MUDA HUU

Image
'tumia vizuri muda huu maana unaweza kukutana na swali gumu baadae halafu ukakosa jibu sababu ya uzembe wa kutolitafuta jibu lake ndani ya muda huu' Na. Omar Zongo Muda huu, ndio zawadi pekee ya manufaa iliyo mikononi mwako!. hebu Vaa uhusika wa marehemu waliopoteza pumzi zao muda mchache uliopita, waonee huruma na utambue kuwa hauna muda wakupoteza na yakupasa uutumie vizuri MUDA HUU. Muda huu ni kipimo cha kufaulu au kutofaulu huko uendako, kwa ufupi ni kuwa Muda huu ni madini yenye thamani yaliyo kwenye viganja vya mikono yako. Muda huu utumie sasa kikamilifu, Acha dharau, acha kiburi punguza Hasira na fikiria upya kujenga jumba la furaha nafsini mwako bila kujali nini unapitia na magumu mangapi yanakusonga. Muda huu acha kuutumia kuvuta sigara sababu unayaumiza mapafu yako na itakugharimu baadae, utumie muda huu kwa kufurahi na yoyote aliye karibu yako, humjui hakujui lakini kama kuna uwezekano wakumsemesha kwanjia ya utani hebu fanya hivyo umjenge...