NGUVU KUZIMU& UDHAIFU DUNIANI, IZRAEL NAOMBA TUYAJENGE!

BY, Omar A. Zongo Izrael Mtoa roho nianze kwa kukupa pongezi, hakika Kazi yako umeifanya kwa ufasaha kuzimu kwapendeza! nami niseme Ahsante kwa kunialika karamu hii ingawa umenisimamisha langoni lakini yumkini naona ndani sina kinyongo, nimeridhika na mwaliko wako! Izrael wewe ni jemedari bingwa wakuchagua vizuri maana hafla yaendelea ndani lakini navutiwa na jinsi kuzimu ilivyo pambwa naamini ni kazi ya akili yako kuwachukua wapambaji mahiri kutoka duniani! maandishi yamepambwa kwa umahiri kutambulisha kuwa hii ni NYERERE DAY! Sina shaka aliyeandika maneno haya kwautashi ulimnyakuwa toka duniania ingawa sijui ni ninani hasa! jukwaa la kuzimu limepambwa kwa mbadilishano wa sauti za wanamuziki wa kila aina TX MOSHI kwa mziki wa dance akiongoza wanamuziki wenzake wengi kutoka kongo namuona kwa mbaali PAPA WEMBA hakika izrael umeimaliza dunia kama ikitokea karamu kama hii duniani wakali hawa hawapo tena waliopo wanafanya kawaida sanaaaa. Nasikia kuzimu SIASA yake safi hai...