Posts

Showing posts from September, 2016

SITAKUSAMEHE

Image
Leo nimekuomba uketi chini nikufunulie tena kwa mara nyengine jarada hili lenye kanuni zangu na muongozo muhimu kwa mchumba angu! jarada hili lina kanuni Hamsini jiandae kujua leo nasoma kanuni ya ngapi maana mara ya kwanza nilikusomea kanuni ya Sita niliyoipa jina la NITAKUOA LAKINI SITASAIDIA NDUGU ZAKO! hii leo nimepata mshawasha wakukusomea kanuni ya Kumi yenye kichwa cha habari chenye neno moja tu SITAKUSAMEHE. kubwa na muhimu tambua kuwa nitakuoa kamwe sitaruhusu maneno yangu haya yakumbwe na kimbunga kiitwacho AHADI HEWA. Nitahakikisha nakuoa na nasimamia furaha yako muda wote ndani ya ndoa yetu! ule ukatili wa mwanaume kumpiga mkewe mpaka kumpa chongo kamwe sitauruhusu univae nakunilaghai, ukinikera nitakutandika na maneno yakukuonya na ukiendelea nakucharaza na dua yenye maombi mazito kwa mola wangu nina imani kupitia yeye aibu yakuniudhi nakunikaraisha itakuvaa na utaona haya kunipa mateso mtoto wa mwanamke mwenzio. yote nitayafanya mchumba kuhakikisha unajivunia...

WAPINGA SIMULIZI 2

Image
Wapinga simulizi wanapatwa na taharuki baada ya tukio la ajabu kutokea katika eneo walilokusanyika. mwenyekiti alichomoka kama mshale na hata sijui aliwezaje kumruka katibu wake mtu mwenye sharubu nyingi kuwahi kutokea duniani. wote waliweza kujimudu nakukimbia kunusuru roho zao lkn tatizo lilikuwa kwa mtu mnene kuliko wote waliokusanyika pale. wakati akiwa anajiandaa kuamka ili akamvamie mwenyekiti ghafla akahisi anavamiwa na kitu kizito mgongoni. kitu hiki ndicho kilichozua taharuki eneo lile, kilikuwa ni mithiri ya kinyamkera, masikini bonge wawatu alitoa yowe la woga akiomba msaada. watu wote walishachanguka katika eneo lile ni bonge tu ndio alibaki, hata mkewe hakujali kabisa kuhusu mumewe. alikimbia mbali kabisa kila mmoja alihakikisha anamuacha mwenzake umbali mrefu sio wanawake wala wanaume, sio watoto wala wakubwa, vijana na wazee woote kwa pamoja waligeuka wanariadha. ni bonge tu ndio alibaki anagaragara pale chini huku lile zigo mithili ya kinyamkera likiwa l...

CHIZI MAFANIKIO SEHEMU YA 3

Image
ILIPOISHIA..... _Mama yake Salim anaingia chumbani kumsalimia mwanae anamkuta amelala usingizi wa kifo, hakutaka kuamini kabisa kuwa Salim amefariki lakini ukweli ulikuwa huo maana hakuweza kuamka hata walipofanya juhudi zakumuamsha_ SASA ENDELEA... Haikuwa rahisi kuamini kuwa Salim amefariki dunia, maswali mengi magumu yalikatiza kichwani mwa mama yake.. wengi ilibidi waamini kuwa labda chanzo cha kifo chake ni kushambuliwa na Jef, hata walipoufikisha hospitali mwili ule wa marehemu hakuna kilichobainika kumuua Salim. ukweli wa kifo ni ukweli ambao hakuna ambaye yupo tayari kuukubali hasa aliyekufa awe na mahusiano ya dhati nawewe. Salim alikuwa ni kijana mdogo sana umri wa miaka 27 pekee anafariki ndani ya siku nne tu tangu atoke uingereza kusoma. wengi waliguswa na msiba huu lakini Bi Getrude aliguswa zaidi, aliamini chanzo cha kifo cha kijana yule ni mwanae Jef. alilia sana na aliumia pia. alishiriki kwa hali na mali katika msiba wa Salim na alionekana kuguswa za...

WAPINGA SIMULIZI :1

Image
Idadi kubwa ya watu wake kwa waume, wazee kwa watoto, wasichana kwa wavulana. eneo ni porini ni nyasi tu ndio zimesambaa kote, watu hawa wamekaa chini ya mti wa muembe. mwenyekiti wa mkutano wao alikuwa ni mfupi kuliko wote waliokuwa pale. alivaa koti kubwa kuliko kimo chake, hakuwa na kipaza sauti hivyo alilazimika kuipaza sauti yake isikike kuwafikia watu wote waliokusanyika pale. watu wakiwa makini kumsikiliza ghafla jamaa fulani ambaye mwili wake ulikuwa mkubwa (mnene) akasikika akipumua kwa nguvu jambo lililozua tafurani na watu kuguna nakupoteza umakini wakumsikiliza mwenyekiti wao. hali ya hewa ilibadilika ghafla katika eneo lile, jamaa bonge huku akiona aibu akajikuta akijikaza kuamka ili aombe radhi lakini kabla yakufanikisha zoezi hilo alijikuta akipumua tena mfululizo tena kwa sauti kuu iliyopenya masikioni mwa wote waliokusanyika pale, masikini ya Mungu mtu mnene yule sijui alishiba maharagwe mpaka yakamfanya ashindwe kujizuia kupumua hovyo nakuharibu hali ya h...

CHIZI MAFANIKIO: SEHEMU YA PILI

Image
Ilipoishia...  Jef anamvamia nakumuangusha Salim huku akimshambulia vibaya, watu wanazunguka eneo lile wakishangaa bila kutoa msaada_ sasa endelea..... Haikuwa rahisi kwa Salim kujinasua pale chini, Jef alimdhibiti 'barabara' na asiweze hata kufurukuta. "Ni miaka mingapi imepita tangu uingie mkataba na kampuni yangu? ulidhani utanitoroka milele, leo nimekukamata utanitambua! umeitia hasara ya mabilioni kampuni yetu!." haya ndio maneno aliyokuwa akiyasema Jef huku akimshambulia Salim. watu waliofika eneo lile waliposhuhudia damu zinaruka ndipo walipopatwana taharuki lakini wengi wao waliogopa hata kusogea karibu mpaka alipojitokeza kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la mtaani Kinongo ndipo akajitosa kumzuia Jef asiendelee kumshambulia Mwenzie. "we Jef nini unafanya!? pumbavu!. hebu muache mwenzio" alipaza sauti Kinongo huku akipata ujasiri wakumsogelea karibu Jef. ajabu Jef hakuwa mbishi ghafla aliacha kumshambulia Salim akanyoosha m...

CHIZI MAFANIKIO ; SEHEMU YA 1

Image
 MTUNZI :  BIN ZONGO Jina Lake aliitwa Jef alikuwa ni mrefu kwa kimo umbo lililoshiba na sura yake haikuwa ya mzaha . Maisha yake yalikuwa mtaani, nguo zake zilimtambulisha kwa yoyote kuwa hakuwa timamu kiakili. alizoeleka kuongea peke yake na kujichekesha mwenyewe bila sababu ya msingi. alikuwa ni mwendawazimu lakini uzuri wake hakuzuru watu wala kugombana nao yeye alipenda kuwachekea na kila gari na nyumba nzuri aliyoiona alijinasibu kuwa ni ya kwake. alipenda sana kuzungumza na watoto wadogo ambao wengi walimzoea jef nakumfanya rafiki. bila shaka wazazi wa watoto wale walithibitisha kuwa Jef hakuwa mwendawazimu wakudhuru watoto ndio maana wakawaacha watoto wao wacheze nae kutwa nzima ingawa pia walikuwepo wazazi waliokuwa wakihofia kuwaacha watoto wao na Jef. wakihisi kuwa ipo siku atazidiwa na uchizi awafanye kitu kibaya. Pengine labda isingekuwa Rafiki yake jef aitwae Salim hata pia nisingepata lakusimulia kuhusu Jef. ni Salim ambaye alijaribu kuelezea ...

UJUMBE WA YATIMA

Image
Tumefanikiwa kuwatembelea wadogo zetu(YATIMA) Ni wenye furaha na amani yaani kwa mara ya kwanza tupoziona sura zao mioyo yetu ilipiga magoti kuwaombea kwa MUNGU wasimamizi wa kituo kinachotumika kuwalea. tumefanikiwa kuzungumza nao nakubadilishana nao mawazo watoto hawa na kwa usiri nafsi zao na zetu zikafanya kikao chasiri. kikao ambacho hakikuhitaji kadamnasi ya watu, na kiliweza kutumia dakika 120 pekee kufika tamati. Baadhi ya watoto yatima wanaolelewa katika kituo cha Tatima Fund Group katika picha ya pamoja na Vijana kutoka Katika Simulizi zinaishi Blog nafsi zao zilipata uhuru kuzungumza mengi katika kikao hicho lakini mwisho zilitupa ujumbe tuufikishe kwa hadhira ya watu ambao ni wanajamii. ujumbe ambao ulianza kuzungumzwa na mtoto mdogo umri miaka saba nakujazwa nyama za maneno nakaka zake aliokutana nao katika kituo kile wakiwa na jina la YATIMA. anasema ndoto ya mafanikio ni sehemu inayoishi ndani yake na inakuwa kila uchwao ikijenga tamaa ya siku moja k...