Posts

Showing posts from August, 2016

BURIANI BI SHAKILA

Image
Hakika kila mmoja anaweza sema lake kuhusu ujumbe huu! ila mimi sitajibu hayo yote nitajibu kuhusu huyu atakayesema kwanini nimechelewa kuomboleza na hata kutia neno kuhusu kifo chako mpaka siku kadhaa sasa zimepita. Burian Bi Shakila na hakika wanazidi kuniliza hawa waja kwa swali hili na kabla sijaendelea kukuaga acha nisemezane nao hivi Ningewazaje kutia neno katika msiba mzito kama huu, msiba uliogonga moyo wangu nakunipa ganzi katika viungo vyote hasa ulimi unaomfanya mtu atamke. ni mikono hii ndiyo iliyoshindwa kabisa hata kunyanyuka nakuipungia mkono wa kwaheri nafsi ya Nguli huyu wa Muziki wa taarab iliyokuwa inapaa angani taratiibu huku ikisonona kuona Taarab asilia waasisi wake wanaisha katika ulimwengu huu. ni macho haya yakwangu Bin Zongo ambayo yalishindwa hata kudondosha chozi ilhali moyo ukiwa umetota kwa huzuni ya msiba ule, hakika yalikuwa maajabu mpk jicho kushindwa kulia kwa mshtuko wa habari hii yatanzia. kama viungo vyangu vilishtushwa na msiba ule nin...

UNATAKA KUJA DAR?

Image
Natoka zangu mihangaikoni, mwili umechoka akili haifanyi kazi ipasavyo nahitaji kuoga nakupumzika, nawaza ningekuwa na mke nyumbani angalau ingekuwa afadhali nipate tulizo walau lakupokelewa furushi langu zito lenye vifaa muhimu vya ujenzi. kazi yangu mie ni ujenzi wa nyumba. sikusomea kazi hiyo bali nilijifunza tu kwa wataalamu wa fani hiyo, nakutokana na utundu wangu nikawa fundi mzuri wa nyumba. ingawa ilikuwa yaniuma sana ninapobaini kila nyumba nzuri inayosifiwa jijini dar es salaam ni kazi ya mkono wangu ilhali mwenyewe bado naishi nyumba yakupanga.  niliwahi jaribu kununua kiwanja maeneo ya chanika nijenge lakini sunami la dhulma na dhoruba kali ya utapeli ikanirudisha nyuma sana. mpaka leo mimi ni mdau wakupanga huku tabata matumbi, maombi yangu siku zote ni mvua isinyeshe maana adha ya maeneo haya aijuae ni MUNGU. unataka kuja?? hatua zangu za kichovu hatimaye zikagota katika mlango wa chumba changu.. naufungua naingia ndani, chumba chanizomea maana tangu ni...

JIANDAE KISAIKOLOJIA

Image
Nina uhakika wenzio yalivyowakuta walihangaika sana nakuteseka sababu hawakujiandaa kisaikolojia. nakuasa mapema sana ujiandae kisaikolojia ndugu yangu maana dunia hii huzunguka kwa usiri katika muhimili wake. mzunguko wake mmoja ni mengi yanajiri na katika hayo mengi naamini kuna moja ambalo linakupasa ujiandae nalo kisaikolojia. we jiandae tu usichoke kufanya hivyo maana muda sio mrefu nimetoka kumbembeleza rafiki yangu aliyeumizwa vibaya na mpenzi wake. anasema "alikuwa akinipenda sana, alinijali mno, hakuwa tayari hata siku moja kuona nasononeka, nateseka wala kuhangaika. mara zote aliniambia hataki kuliona chozi langu, nilimuamini na sikuwahi kudhani kama angenifanyia haya" huyu ni mfano wa mamilioni ya watu duniani ambaye anaumia nakulia sababu hakujiandaa kabisa kisaikolojia yeye aliamini mapenzi aliyopewa hayatakuja kubadilika. nina uhakika angejiandaa mapema kwa kujua kuwa mapenzi ni kama majira ya mwaka hii leo asingelia maana tahadhali tayari angekuwa a...

AHSANTE MWANA KUJA

Image
Nakushukuru Karima, umpendevu ajabu Unanifanya nahema, kunipa nyingi thawabu Ninaipata salama, sia yakutu bawabu   Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata Ikarima ya Imamu, shauku   tunu amini Ulinipatia salamu, kwa mikonoko kichwani Ukaniita binamu, na majina ya utani   Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata Umenialika kwako, nakuja nafamilia Nabeba yangu   mifuko, na vibwende navalia Usije pata shituko, mi sina cha kulalia   Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata Una nyumba kubwa sana, tarifa nimepata Yenye viwanja vipana, na kwa kufugia bata Nina kuweka bayana, usipike vya mafuta   Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata situmii vya dukani vinanitoa malenge Sijapona na   madonda, nilopata mwaka jana Hapa nipo nimekonda, mzee kama kijana Pika ninavyo vipenda, vya enzi zetu za jana   Ahsante mwanakuja, salamu nimezipata Situmii vya dukani, vinanitoa malenge Andaa na vya zamani, kama vya kwa...

Waandishi Wanaandika

Image
sijui hata wanakuwa wapo wapi muda huo wakiandika! wanaandika kwa utashi na weledi wa hali ya juu, huandika kila aina ya jumbe tena kwa mpangilia kuntu unaoeleweka na usio msumbua msomaji.. Mwanzo wa maandishi yao hupamba kwa maneno yenye mvuto yanayompa kila sababu msomaji aendelee kusoma. kwa hakika watu wanaandika! navutiwa kusoma maandishi yao na hua natenga muda wangu kuyasoma maana hunipa maarifa maandishi yao! kila niendeleapo kusoma nagundua kuwa utashi wa watu kuandika kuhusu KUTOKUKATA TAMAA YA MAISHA unaongezeka. kila mmoja huvaa uhusika wa mueleweshaji wa wengine kuhusu kutokukata tamaa na magumu tuyapitiayo! nafarijika sana kuona aina hii ya maandishi sababu saikolojia za wasomaji zinazidi kuamini kuwa kukata tamaa ni sumu ya mafanikio, nami nisisitize TUSIKATE TAMAA!. Maandishi haya zaidi nayaona kwenye mitandao ya kijamii na watu wanashare kwa nguvu kuonesha nia yakusaidia wengine wasome. Maandishi mengine ni kuhusu MAHUSIANO utakuta maandishi mareefu...

KUMBUKUMBU YA PENZI

Image
Nilikuita jina gani, kwanza nilipo kuona Nilianza kwa utani, au nilijua jina Hivi ilikuwa sokoni, au kwa kina Safina Moyo wangu umetuwa, kumbukumbu we rejea Nilianzaje kusema, kwa binti wewe mrembo Ni kweli sijatetema, kwa mvuto wako wa umbo Ni vipi je nilihema, kwa tenzi zangu za fumbo Moyo wangu umetuwa, kumbukumbu we rejea Jicho lipi shahadia, jasiri kwa babu babu Nilijawa na hisia, kisio lenye sababu Nilianza simulia,   ni kipi kilinisibu Moyo wangu umetuwa, kumbukumbu we rejea Au nilikusifia, pasipo kunjo aibu Hivi nilikurukia, tena pasipo adabu Wewe uliye malkia, mrembo usiye gubu Moyo wangu umetuwa, kumbukumbu we rejea Sikumbuki ilikuwa lini, na jibu gani ulinipa Ila nipo furahani, nisiye penda kwa pupa Nimekuweka moyoni, nihifadhi kwenye chupa Moyo wangu umetuwa, kumbukumbu we rejea Penzi hili si kasiri, Kaharu kalipangia Tena halina tafsiri, kwa jina kulipatia Tuijenge tafakuri, magumu tukipitia Moyo wangu ume...

ZIMETOSHA SIFA ZENU

Image
Nimesema Sitaki Misifa Ndio sizitaki sifa zenu na kwa kauli nyengine ningesema Sitaki tena kusifiwa, kama ninyi ni mahodari wakusifia mpeni sifa jogoo ambaye ana juhudi kubwa yakuwaamsha alfajiri ili mkatafute riziki. mimi sitaki kabisaa sababu MUNGU wangu alinipa upeo na busara yakutambua jema na baya. kuhusu sifa mnazotoa sioni wema hapo nauona ubaya, naomba msinisifie tafadhali. kama mna nia nzuri na mnataka mema kwangu fanyeni maombi ili bendera ya SIMULIZI ZINAISHI iendelee kupepea vema. mkifanyacho sasa mnarusha mawe yalio na mfano wa mkate yanatua sawia kichwani mwangu maumivu na kuvimba kichwa hiki yatasababisha nisiwe msanifu na mwenye kujiongeza tena. kwani ni wangapi walioanza vema wakasifiwa kwa nderemo na vifijo na matokeo yake wakapotea mithili ya jua majira ya jioni. Sitaki tena sifa zenu! naamini kuwa sifa hizo ndizo zitakazonifanya nifanane na wengine waliowika Tanzania hii. wale ambao waliweza kusahau utamu wa lugha yetu wakaweza kuhadaika na kua...

MIMI NI NANI?

Image
Mimi Ni nani "hii simu nani kaiwasha!?" maneno haya yalijisema yenyewe ndani yangu huku uchovu wa usingizi unaomalizikia ukiwa umenizingira kote maungoni mwangu. ilikuwa ni asubuhi, dirisha lilipenyeza miale ya jua la asubuhi, jua ambalo liliwika kama jogoo likiwataka watu waamke kuutafuta mkate wa kila siku. ilikuwa ni jumaapili tarehe sikumbuki wala mwezi pia kwa hili nakiri kuwa kweli mimi ni kilaza! sauti iliyojisemeza ndani yangu ikiilalamikia simu ilitokana na mlio wa simu hiyo kunitoa katika ladha taaamu ya usingizi wa mwisho wa wiki. huku nikijigalagaza kivivu kwenye uwanja wa fundi seremala nikaurusha mkono wakulia ambao uliifikia simu ile lkn bado swali lilikuwa ninani ameiwasha maana sikuwa na kawaida yakulala nikiwa nimewasha simu. lakini sikuendelea kuumiza kichwa kuwazia hilo sababu pia sikua na uhakika kama jana yake nilikumbuka kuizima. kono langu la kulia lililofura uvivu tayari liliikamata ile simu kibabe na kuisogeza usawa wa uso wangu sa...