Posts

Showing posts from June, 2016

Shaaban Robert Katabasamu

Siku kadhaa zimepita tangu niandike barua kwa marehemu nguli wa Kiswahili na mtunzi wa mashairi Sheikh Shaabani Robert, Usiku naweweseka nashtuka nakiona kivuli cha  Shaaban Robet, kinanikabidhi Barua, kisha kinatoweka machoni mwangu , napigwa na butwaa, nakurupuka kana kwamba nimemwagiwa maji ya baridi naikimbilia taa naiwasha , mkononi  mwangu nauona  waraka ule wa barua niliyokabidhiwa, moyo unaenda mbio, macho yanakimbilia kusoma kilichoandikwa! Maneo ya juu kabisa yameandikwa. Shaaban Robert Katabasamu! Naongeza umakini kusoma zaidi…. iliandikwa hiviii. Asante sana, kilembwe changu, yumkini baadhi ya kizazi chenu chatambua niliwahi kuwapo duniani basi  najifaghiri sana huku nilipo. Barua yako nimeipokea, ingawa hukuipa jina barua ile ila nikaona nisifanye kosa kama ulilofanya wewe  yakwangu mie nimeipa jina hilo hapo juu, Shaaban Katabasamu. Kwa hakika umenifanya nitabasamuj kwa mara ya kwanza tangu kufariki kwangu, mwanzoni niliv...

Mafanikio Yatabaki Kwao!

Image
Nafsi za wazee wao zinacheka kicheko cha majivuno, wanajivunia sana kuacha vizazi  ambavyo vinaenzi uwepo wao, sura za wazee wao zimepambwa na tabasamu wanagonga  glasi zao za mvinyo kwa furaha na hawaachi kubariki harakati za damu zao zinazoendelea kupumua na kuitumia hii hewa ya bure kabisa ambayo Mungu aliamua ujira wake uwe ni kumcha yeye tu. kwa hakika mafanikio lazima yawe kwao. hata kama ugumu upo wakuyafikia mafanikio lakini kwao ugumu unageuka kuwa ulaini, ulaini ambao unatokana na furaha na amani ya wazazi wao kutokana na kuenziwa kwa juhudi zote nakutangazwa kwa michango yao katika historia ya waliopo sasa na hata wa kesho, lazima wafanikiwe. najua busara zi pamoja nawe na ndio mana unasadiki kuwa mafanikio yataendelea kuwa kwao sababu hata makazi ya wazazi wao ya milele bado yangali na thamani na wanayaenzi kwa marefu na mapana, sasa kuna kipi kinaweza fanya laana ya umasikini iwe kwao! nasisitiza ni lazima wafanikiwe! tutaendelea kutamani kutibiwa kwao, kula...

Kuanzishwa, kuishi na kuanguka kwa Taifa Daladala!

Image
Taifa lenye kila aina ya sifa lakuitwa taifa lenye maendeleo, ajabu haliishi mtu ndani yake, limeumbwa kwa mvuto wa hali ya juu, linavutia ndani na nje, kwa upande wa nje limechorwa maandishi makubwa mbele, maandishi yaliyonakshiwa kwa rangi za bendera ya tiafa hilo, maandishi hayo yanasomeka DALADALA. Watu wawili wanaonekana wakishangaa uzuri wa taifa hilo, wanastaajabu kwanini taifa zuri kama hilo haliishi watu, wanalisogelea, wanalikagua mwisho wanaambizana Daladala             ''tunaweza kuwa viongozi wa taifa hili, tutawakusanya wananchi mbalimbali kutoka maeneo tofauti ya dunia nakuwafanya wawe raia ambao wataishi ndani ya Taifa hili kwa kulipa kodi maalumu, inapoisha wanaachana na taifa letu tunatafuta raia wengine, hii itasaidia kuongoza nchi hii sababu ikitokea hata tunatakiwa tukarabati miundombinu na makaazi ya watu inakuwa ni rahisi kutumia kodi zao'' wanaweka mikakati, kanuni yakuendesha Taifa hilo, wanaridhika mmoja anajipa madaraka y...

WEWE,

Image
Sio kosa kukunyooshea kidole wewe hii leo, nakumbuka niliwahi kukemewa kumnyooshea kidole mtu yeyote ama awe mkubwa kwangu au mdogo lakini leo sitakiweka chini kidole hiki nitakinyoosha kwa uthabiti tena bila kutetereka , nakunyooshea wewe kidole hiki. Sio fahari hata kidogo na huwezi sifiwa kwa tabia zako za ubinafsi, choyo na uzandiki, hufai kwa kulumangia wala kulia na kachumbari, ni wewe ndio nakuwambia, unajisikiaje kuishi kifahari kama mfalme ilihali waliokuzunguka ni dhalili, wamechoka na macho yao yanaongea shida na ufakiri uliowagubika.  Eti wewe? Kwani wewe ni nani hasa katika hii dunia mpaka watoto wa wenzako uwageuze punda kwa kuwabebesha madawa yakulevya na kuuza utu wao? Eti wewe ni nani? Nani amekwambia kama dunia hii ni yakwako na kwamba una haki yakutesa wenzako sababu ya pesa? Wewe Kidole hiki kina beba mengi na labda tu nikwambie huwezi kukikata licha ya kwamba unamiliki kila aina ya ,kifaa cha kukatia utu wa wenz...

Nimepata Nafasi.

Image
Sitaki ifike sehemu nikukose eti kisa sijaitumia hii nafasi, nakumbuka vizuri kuna siku fulani niliwahi kupata nafasi kama hii..ulifurahi sana ukapata sababu za kuwa namimi karibu, ukanipenda sana, ukaniamini nakunipa dhamana yakuubeba nakuutunza moyo wako. umepita muda mwingi sana sijarejea tena nilichoongea siku ile, nina imani utakuwa umekumbuka sana na unatamani hata siku ile ijirudie, nitakuwa mkosefu sana nikiendelea kukuacha utamani ule muda ilihali mimi ningali hai! acha niutumie muda huu sasa, kukwambia tena maneno sawa na niliyokwambia siku ile, Sikuwahi hata siku moja kujua maana ya kupenda kabla sijakutana nawe, nilikuwa nabishana na waliowahi kupenda hasa walipokuwa wakidai kuwa maumivu ya mapenzi yana uhusiano na moyo,  niliwabishia enzi zile sababu sikuwahi kuona hata siku moja moyo wangu ukipatwa na msukosuko eti sababu ya mapenzi! wapo waliosema kuwa mimi bado sijapenda nikawaambia nimependa sababu enzi zile alikuwepo wapembeni yangu lakini ukweli nikwamba haku...

Barua Kwa shaaban robert Kwa video

Ikiwa imepita miaka hamsini tangu kufariki kwa nguli wa mashahiti na mtunzi wa simulizi mbalimbali Baba wa kiswahili Marehemu Shaaban Robert, hii ni barua ambayo tumemuandikia ili kuenzi kazi zake na juhudi zake zakuipa heshima lugha yetu, Itazame Barua hiyo katika video hii

Barua kwako Mzee wangu Shaaban Robert

Image
                Salaam ama baada ya salaam, Ni matumaini yangu umelala pema peponi, naamini hivo na naendelea kumuomba Mungu aendelee kukupa pepo sababu ya mchango wako mkubwa wakusimamia nakuipa heshima lugha yetu ya kiswahili nakuinyoosha jamii kupitia kipaji chako adhimu ulichokuwa umejaaliwa,                          Umezaliwa miaka ambayo sio mimi tu hata baba yangu na mama walikuwa hawana dalili yakuzaliwa, lakini nalipa heshima sana tukio lakuzaliwa kwako,ilikuwa ni zamani sana, zamani isiyosemeka, zamani ya mwaka 1909. nalipa heshima tukio lakuzaliwa kwako sababu zikiwa ni nyingi lakini kubwa ni heshima uliyowahi kuiwekea nchi yangu pamoja na lugha yangu ninayoitumia, kwa dhati ya moyo wangu kabisa napata muongozo kupitia wewe ingawa sijui ni muongozo gani sababu umefariki kipindi ambach...

Nitaomba muda wako 'Uisome'

Image
Baadhi ya vitabu vyenye upekee wa Shaaban Robert katika uandishi Kama utakosa kabisa muda basi tafadhali naomba niazime hata ule ambao unautumia kwa kunywa maji, laa kama huo pia utasumbua tafadhali sana naomba ule muda unaotumia kupokea simu ya umpendae, kama hiyo ngumu basi hata ule muda ambao unatumia kumeza mate tu, naahidi sitatumia muda mwingi sana kidogo tu nitakamilisha ninachotaka unisaidie, Unamfahamu Shabani Robert, moja ya binaadamu waliowahi kuishi duniani ukanda wa afrika mashariki, alikuwa ni mfano wa lulu kutokana na utashi wake wakubuni kuandika mashairi na simulizi mbalimbali zenye kufunza na kwa hilo mitaala ya elimu yetu tanzania inajua umuhimu wa huyu mzee katika kufundishia lugha na fasihi simulizi kwa ujumla, Ni heshima kubwa aliipa nchi yetu na bado hadi hivi leo kumekuwa na juhudi mbalimbali zakulienzi jina la Nguli huyu.. kama ingekuwa utashi na kubuni visa mbalimbali vyenye kuonya, kukosoa nakuelimisha ni kibali chakuishi milele sina shaka hadi hivi...

Acheni Niandike

Image
Nchi inaitwa WATAJIJU serikali yake inayoongoza nchi hii ina nguvu na inafahamika kote ulimwenguni ikiitwa WAPUUZAJI  watumishi wa nchi hii wote hujitambulisha kwa sare zao zenye nembo hiyo, WAPUUZAJI. Miongoni mwa vijana waliozaliwa nchini humo  mmoja anakibaini  kipaji chakuandika lakini  kabla yakuanza kuandika anajikuta anarejea historia ya waandishi waliowahi kupita katika nchi ile, Naam! anajifahiri sana, anajikuta kuwa hayupo peke yake waliwahi kuzaliwa vigogo na manguli katika sanaa aliyoigundua kuwa ipo ndani yake, lakini katika kufuatilia historia za waandishi hao, simanzi inamkaba...wengi anaona kazi zao nzuri huku wanahistoria wakisifia uhodari wa waandishi hao wengine wakidiriki hata kusema namna ambavyo wamechangia kukuza lugha adhimu ya taifa la Watajiju, wananchi wa taifa hilo wamegawanyika kwa makabila tofauti lakini asilimia kubwa waliweza kuongea lugha ya taifa lao iliyoitwa TWAIZARAU, Lazima Niandike Asilimia kubwa ya vitabu vilivyowa...

Inataka Moyo

Image
sio rahisi hata kidogo na inahitaji moyo na sio mradi moyo tu, moyo wenye ujasiri na usio mwepesi kutiririkwa na machozi, moyo wenye kustahimili na wenye kuelewa kuwa haya mambo ndivyo yalivyo na yanahitaji utashi na busara ili yaweze kukupa heshima kwa vizazi vyote vya sasa na vijavyo, Waswahili walitukuka kwa misemo na walimaanisha waliposema ukiona vyaelea ujue vimeundwa, au ukitaka uzuri sharti uzurike. Inataka Moyo walikuwa na maana pana sana waliposema hayo lakini maana hiyo ililenga hasa maisha yetu ya kawaida. Umezaliwa Kijijini hakuna nyezo za aina yoyote ile, shule ipo mbali sana inasababisha hata viatu vya shule visidumu nakufanya muda wote vionekane kama vinacheka mbele na soli ikiwa ina upara wa lazima unaotokana na kiguu na njia kila uchwao. unajikuta una uwezo mkubwa wakuimba lakini kipaza sauti hujawahi hata siku moja kukiona, wenzako mjini wanatunga mashairi huku ala ikiwa inasikika aidha kwenye kinukulishi, au simu lakini wewe huna hata redio, baba ...

NITAKUOA LAKINI SITASAIDIA NDUGU ZAKO!

Image
Mchumba hili ni neno la sita katika kitabu changu   cha vitu ambavyo unapaswa kuvijua kabla sijakuoa, Ni neno la sita lakini nimeanza nalo kutokana na umuhimu na pia lina fitina sana neno hili maana wabaya wetu wasio penda mahusiano yetu lazima watakwambia kuwa mimi mume gani, nina roho mbaya na sifahi kukuoa sababu ya neno hilo, Mengine yaliyopo katika kitabu hicho   na wala usilalamike kuanza na neno la sita sababu tayari nimeshakwambia hapo juu mchumba, utayafahamu Acha nikufafanulie ili wanafiki, wafitini wasipate kutumia neno langu hilo kunigombanisha nawe na mwisho tukaachana , Kwanza fahamu kuwa nitakuoa hilo ni lamuhimu sana na unapaswa kulijua, nafanya kila liwezekanalo na tayari nyumbani kwetu wameshajua, wazazi wamebariki wananingojea mimi tu, lazima nitakuoa mchumba tuseme ishaallah, Lakini mchumba, kabla sijakuoa naomba ujue na utambue kabisa kuwa sitasaidia ukoo wako, nitakachofanya mimi nitahakikisha unakula vizuri unalala vizuri, unapata kila ...

Ni Kama Nyota

Image
Majira yanabadilika, kuna muda anga linameremeta kwa uangavu wa jua, huku likiwa na matokeo ya joto kali na mvuke wa moto utokanao na hasira za kuwaka kwa jua hilo! sijui lakini naamini kuna maana ya jua kuwaka mchana na watu kuhitajika wafanye kazi mchana ili kukamilisha ule msemo usemao, mtatafuta kwa jasho, ikiwa na mantiki ya kwamba hata kama kazi yako itakuwa ya kukaa tu, lakini kutokana na ukali wa jua lazima jasho likutoke labda kwa wale wenye viyoyozi katika maeneo yao ya kazi, lakini muda wote jua halitishwi wala kubabaishwa lenyewe linawaka tu na ukithubutu utoke nje utakutana nalo!. lengo sikulisakama jua, la hasha! lengo langu nikuzungumzia majira yanavyobadilika, kuna muda ukitazama anga utagundua kuwa halipo tena jua, giza linakuwa limetanda kote na anga lote linapambwa na vimeremeta vyenye kupendeza na huwa vingi sana angani, na kama ukivitazama kwa hisia kali lazima neno litakutoka, neno lakupongeza kazi ya MUNGU. kazi ambayo hufanyika kwa siri kubwa hivyo k...

NILIWAHI

Image
Niko ndani chumbani, ugenini,gizani, najihisi mpweke, aliyezima taa sijakua nae, simjui nimekutana nae ukubwani, nakumbuka utotoni niliwahi kuzoeana na mtu kama yeye lakini sio yeye, nabaini kuwa kila siku iitwayo leo hili neno niliwahi linaendelea kunizoea sababu naweka historia ya mambo mengi ambayo nayapitia Nakumbuka vizuri kabisa kuwa niliwahi kuwa na wazazi, baba na mama yangu, alianza kufariki baba nikabaki na mama na mara zote nilikuwa najiambia kuwa niliwahi kuwa na baba, maisha yameenda sana hii leo sina mama, najiambia tena kuwa niliwahi kuwa na mama sababu sipo nae tena, Niliwahi kulia nakubembelezwa kwa upendo huku nikiulizwa unataka nini mtoto, lakini sasa hivi imebaki simulizi tu na huku nikijiwazia mwenyewe kwa kusema kuwa niliwahi kupitia maisha hayo, Niliwahi kuwa na ndugu zangu walinijali kama mdogo wao, kipindi hicho nasoma walihakikisha sikosi kitu na walinitetea pale nilipokuwa naonewa, lakini sasa hivi imebaki kumbukumbu tu  na nakubali kuwa kipindi ki...

TAFITI NDANI YA SIKU HATARI......

Image
Nilitamani sana kupata mke mwema, hasa atakayeweza kusimamia familia yetu hata kama Mimi ikitokea sipo duniani. Nimewaza mambo mengi sana ikiwemo namna yakumpata mke huyo, KUCHAGULIWA MKE NA WAZAZI mnh!! Hapana kwakweli sababu Mara kadhaa wao wenyewe wakikawazana wanaropokeana KWANZA ISINGEKUWA WAZAZI NISINGEKUWA NAWEWE sasa ina maana gani niwape dhamana wanitafutie mke ilhali wenyewe wanajutia. kitu pekee nilichoona ni sahihi nikufanya utafiti wa Nani wa kumuoa kitu kizuri nikwamba kumbe sio Mimi tu niliyeanza kufikiria suala hili Wapo vijana wengi sana na wengine ni watu wazima hawajaoa bado wanafanya tafiti....  Lakini naanza kubaini kuwa njia yakufanya tafiti ni hatari sana sababu ili tafiti ikamilike na umpate wa sahihi inabidi ukae kidogo na mtoto wa watu! Utaanza urafiki wakuzawadiana cake na maneno mazuri kwenye birthday mwisho kukaribishana ndani kutazama movie, mwisho ukaribu usio na mipaka na mwisho kabisa majina yanabadilika wanaitana hubby, love, bae na maji...